You Can Win If You Want

Fanya hivi kuzuia hali ya kukata Tamaa

Kuzuia hali ya kukata tamaa ni kitu cha msingi na kinachosaidia kufikia malengo yoyote uliyonayo

Kukaa tamaa ni hali ambayo humkuta kila mtu hasa anapokuwa katika utekelezaji wa malengo makubwa

Kuna muda mambo huwa magumu sana na mtu huamua kuacha anachofanya

Hivo leo ntaongelea namna ya Kutokukata tamaa ili kufikia mafanikio kwa kukupa siri Moja kubwa

Katika harakati za maisha ya kila siku kuna muda tunakutana na changamoto za aina mbali mbali ambazo wakati mwingine hupelekea kukata tamaa na kuelemewa kwa mawazo na hata kufikiria kuacha kile tunachokipambania

Jifunze kuzuia hali ya kukata tamaa

Lakini unapaswa kupambana mpaka mwisho na kuona matunda ya jambo unalo pambania iwe elimu, biashara, kazi, kipaji au jambo lolote lile

Hakikisha kuwa haukubali kurudi nyuma mpaka pale utakapoona faida ya jasho lako.

Kuzuia hali ya kukata tamaa

Tafuta Sababu Ya Kuendelea na zuia hali ya kukata tamaa

Wakati mama yangu anapigania uhai wake wa mwisho aliniita na kuniambia

mwanangu kwa hali yangu ilivyo najua siwezi kupona na sina urithi mkubwa wa kukuachia zaidi ya neno moja tu kuwa “SOMA SANA” hata kama ndugu wasipokusaidia hakikisha unatafuta namna ya kusoma na usikate tamaa”.

Baada ya mama yangu kufariki kitu pekee nilichobakinacho ni Kauli yake,

Kauli ile ilijirudia akilini mwangu mara kwa mara na sikukubali kuacha masomo hata pale nilipokosa msaada kutoka ndugu wote

Niliamua kutafuta kazi ya kuniingizia kipato muda wa nje ya masomo na haikuwa rahisi kwani Ndio kwanza nilikuwa kidato cha tatu tu

Hali ilikuwa ngumu sana maana sikuwa na uhakika wa chakula, vifaa vya shule, ada wala mahala pa kuishi

Lakini kwasababu nilikuwa na nia ya dhati na hamasa ya maneno ya mama sikukubali kushindwa kabisa

Mambo yalikuwa magumu sana lakini nilijitahidi mapaka nikamaliza elimu ya chuo kikuu,

Ila mpaka sasanina amini kama yasingekuwa maneno ya mama basi kamwe nisingeweza kuendelea na masomo.

Angalia hamasa yako upya

Najua umekata tamaa na Huna nguvu za kusonga mbele, lakini nakuomba usiishie njiani

Jiulize kwanini ulianza kufanya unachokifanya na kwanini unataka kuacha ikiwa hujafikia lengo lako

Fikiria furaha utakayopata baada ya kutimiza malengo yako na majuto utakayopata kama ukiishia ulipo sasa, Ninaamini sio rahisi Ila unaweza

Hebu tamaza nyuma na kisha angalia hamasa yako upya, ongeza hamasa na simama katika mkazo wa nguvu na utaona namna utakavyopata matumaini mapya.

Pia soma mafanikio

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Alama za Nyakati Na Mafanikio

Next Post

Imani ndio siri ya mafanikio

Acha Comment Yako

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.