You Can Win If You Want

Wazo La Biashara Ya Genge7 Min Read

biashara ya genge

Utangulizi

Biashara ya Genge ni moja kati ya bidhaa muhimu sana katika matumizi ya kila siku watu kwa wote,

Kwa maana kuwa kila mmoja katika mlo wake wa siku nzima huhusisha mahitaji ya bidhaa za gengeni kama nyanya, kitunguu,mboga mboga,Ndimu nk

Biashara ya genge inaweza kuhusisha pia uuzaji wa mchanganyiko wa matunda aina mbalimbali

Ukiondoa mboga mboga kama mchicha ,matembele,spinachi,sukuma wiki, kisamvu na nyinginezo

Pia unaweza kuuza Samaki, dagaa, viungo vya mboga na vitu vingine vingi kulingana na uhitaji wa watu wa eneo lako na ukubwa wa mtaji.

Wazo la biashara ya genge
Photo by Pixabay on Pexels.com

Biashara hii unaweza kuanza kwa mtaji kidogo sana na kupata faida kubwa kwasababu ni bidhaa ambazo faida inajizalisha

Kujua jinsi ya kuanza biashara bila mtaji kabisa soma hapa

Uzuri ni kuwa soko lake lipo inategemea na ushindani wa eneo na ubunifu wa ziada bila kusahau kipato cha watu wa eneo hilo

Biashara ya genge inaweza kufanyika katika namna tofauti tofauti kama :

Namna Mbali mbali Za Kufanya Biashara Ya Genge

  • Kutembeza
  • Mtandaoni ( derively)
  • Kibandani ( eneo moja)
  • Sokoni
  • Shambani (Bustanini) nk
Kutembeza

Kama huna aibu unaweza anza kwa kutembeza mahitaji muhimu ya bidhaa za genge mtaani , nenda sokoni chagua baadhi ya vitu vichache kama nyanya na kitunguu ,hoho nk

Pita nyumba hadi nyumba tangaza bidhaa zako kwa ushawishi mkubwa ,

Unaweza tembeza kwa mguu, toroli au hata Baiskeli , inategemea na kile kilicho ndani ya uwezo wako!

Mtaji wa kuanza nao hata elfu 10000 au zaidi inatosha kama utaenda kununua sokoni kwa bei ya jumla na anza vitu vichache tu

Ikiwa huna mtaji kabisa ongea na wenye bidhaa uliowazoea na omba wakupe baadhi ya vitu utembeze

Kisha ongeza bei kidogo tu mfano kama nyanya ni 500 fungu wewe uza 600 au zaidi inategemea na kipato cha wanunuaji

Ukimaliza rudhisha mtaji wa watu na wewe baki na faida yako , kisha endelea na utaratibu huo mpaka mtaji wako utakapokuwa

Hapo zingatia Umanifu wa hali ya juu, kumbuka uaminifu ni silaha kubwa sana.

Mtandaoni ( derively)

Maisha yamehamia mitandaoni kwasasa, hivyo anza kujitangaza kisomi kuwa unauza bidhaa za genge

Weka picha nzuri zenye uhalisia , anza na watu wa maeno ya karibu kupunguza gharama za nauli

Ikiwa utapata mteja unaweza mpelekea mahitaji yake kwa nauli yake kama ni mbali na pia unaweza ongeza bei kidogo

Zingatia ubora wa bidhaa zako na wingi wa bidhaa anazotaka mteja , ndio silaha ya biashara ya genge

Mtaji unategemea na kiwango ulichonacho na hata kama huna fanya kuongea na wafanyabiashara wa bidhaa za genge

Hakuna anaekataa kutoa bidhaa kwa mali kauli kama ana uhakika wa kulipwa maana hata yeye lengo lake ni kuuza!

Au fanya kwa namna nyingine yoyote upendayo wewe binafsi kwenye mawazo yako na rahisi kwako jambo la msingi ni kufanya mauzo!

Kibandani

Unaweza pia kufanya biashara ya genge kwa kutafuta eneo moja lenye muingiliano wa watu wengi

Unaweza kuanza na kibanda cha miti na mbao, fremu ndogo au mahala popote rahisi kulingana na mtaji wako

Pia kama huna vyote au uwezo wa kupata eneo basi fanya hapo hapo nje ya nyumba unayokaa

Weka ,meza ndogo na panga bidhaa zako!

Sokoni

Unaweza pia kuuza bidhaa za genge sokoni kwa bei ya jumla au reja reja ukaanza kwa mtaji au hata bila mtaji

Ukiwa na mtaji, kodi eneo kwa bei rafiki anza na bidhaa rahisi kuuzika kama nyanya na vituguu au chagua bidhaa ya aina moja tu

Mtaji unaweza kuwa angalau sio chini ya laki 150000 laki na nusu maana baadhi ya maeneo hukodishwa kuanzia elfu 20000 kwa mwezi

Unaweza anza na malipo ya miezi mitatu au zaidi, pia gharama za kodi zinaweza kuzidi hapo kutegemea na aina ya soko

Uza kwa jumla au reja reja vile upendavyo na kulingana na aina ya soko ulipo mfano wa Dar es salaam soko la jumla ni kama

Temeke stirio, Vetenari, Kariakoo,Tandika,Buguruni sokoni na kwingineko masoko yote haya unaweza uza kwa jumla au reja reja

Kuna wakulima na madalali wengi huleta mahitaji ya bidhaa za genge sokoni na mara kadhaa huwapa wauzaji kwa mali kauli kisha jioni hupitia mauzo.

Ukishidwa kabisa kupata eneo basi kuwa dalali wa bidhaa hapo hapo sokoni kwanza baada ya kupata uzoefu na watu utachukua eneo lako.

Shambani ( Bustanini)

Hapa sasa unaweza kulima mboga mboga au bidhaa nyingine za genge kutegemea ukubwa wa eneo lako

Vile vile ukubwa wa mtaji wako, kumbuka sio lazima uwe kijijini sana hata mjini kama una eneo unaweza panda mboga

Vile vile bidhaa hizi hazitaki muda mrefu sana kuvunwa unaweza anza na bidhaa zinazochukua muda mfupi

Kisha ukafanya mauzo yako hapo hapo shambani au kwenye bustani yako yaani wateja watakufuta

Au hata unaweza kuuza kwa njia nyingine upendayo.

biashara ya genge
Photo by Roman Biernacki on Pexels.com
Vilevile Biashara ya Genge unaweza kufanya katika muundo wa
  • Kisasa au
  • Kizamani

Yote ni namna ya kuipa thamani biashara yako na kupunguza hasara bila kusahau kuongeza mauzo na kuteka wateja.

Mtaji Wa Kuanza Biashara Ya Genge

Mtaji wa biashara ya genge unategemea namna unavyotaka kufanya biashara yako, kwangu mimi hata bila mtaji kabisa inawezekana

Na unaweza anza kwa mtaji kuanzia elfu tano na kuendelea kiwnago unachotaka mwenyewe

Jambo la kuzingatia ni wateja maana sio kwamba ukiwa na mtaji mkubwa ndio utauza sana!

Mauzo yanategemea sababu nyingi sana nje ya mtaji ulionao. Kumbuka kuna tofauti kubwa kati ya mtaji mkubwa na mauzo mengi

Japokuwa mtaji mkubwa ni moja kati ya sababu inayopelekea kuongeza mauzo na kupata faida nzuri,

Lakini kumbuka kuwa biashara ya genge ina faida na hasara kubwa kama ndio kwanza unaanza na huna wateja

Sikushauri kuanza na bidhaa nyingi wala mtaji mkubwa sana , utaongeza mtaji wako taratibu kadiri unavyopata wateja

Kwahio fanya uchunguzi na anza na aina ya uuzaji unayotaka kisha chagua kiasi cha kuanza nacho.

Changamoto Za Biashara Ya Genge Na Jinsi Ya Kuzikabili

Hakuna kitu kisicho na changamoto kabisa japokuwa changamoto huzidiana katika biashara na hata maisha

Moja kati ya changamoto kubwa sana ya genge ni bidhaa kuharibika au kuoza kabisa

Kwa sababu bidhaa nyingi za genge ni zile za muda mfupi kama mboga mboga za majani, nyanya , matunda na hata vingine

Hasa kama ndio unaanza na hujazoeleka sana wala huna wateja wa uhakika

Hivyo basi kuweza kukabiliana na changamoto hii unaweza kufanya hivi

  • Anza na bidhaa chache
  • Uza bidhaa zisizoharibika haraka
  • Nunua friji la kutunzia bidhaa kama una uwezo
  • Hakikisha una tanua soko lako kwa nguvu na kutafuta wateja mara mara usitegemee wateja wale wale
  • Uza kwa punguzo la bei ila zingatia gharama ulizonunulia
  • Kopesha bidhaa ikiwa zinakaribia kuharibika
  • Ubunifu wa ziada ni muhimu kuteka wateja
  • Tafuta eneo lenye washindaji wachache ili kupunguza ushindaji
variety of fruits on fruit stand
Photo by Emma Cate on Pexels.com

Mambo Ya Kuzingatia Kwenye Biashara Ya Genge

  1. Ubunifu

    Hii ni silaha ya kwanza kwenye biashara ya genge , angalia namna ya kuteka wateja warudi mara kwa mara na kufanya mauzo kila siku

  2. Uza vitu vinavyotoka sana

    Unaweza weka vitu vya ziada lakini zingatia mahitaji ya watu ya kila siku na mara kwa mara

  3. Bei nzuri

    Panga bei kulingana na kipato cha wanunuzi na usiweke tamaa ya mfanikio ya haraka

  4. Kauli nzuri

    Zingatia kauli nzuri kwa wateja kumbuka mteja ni mfamle na lazima umnyenyekee

  5. Uchaguzi wa eneo sahihi

    Jitahidi kuchagua eneo lenye mzunguko wa watu wengi sana maana watu ndio wateja wenyewe

  6. Elimu ya genge

    Uliza wajuzi na wazoefu wakupe elimu kabla hujafanya uwekezaji wowote pia kuwa mdadisi mara kwa mara

  7. Nidhamu ya pesa

    Bila nidhamu katika matumizi ya pesa itakua ngumu sana kuendesha na kuendeleza biashara ya genge

  8. Bidhaa nzuri zenye kuvutia

    Epuka kuuza vitu vilivyooza kabisa au kuharibika kwa lengo la kupata faida kubwa, uza vitu sahihi na vinavyofaa kwa matumzi.

  9. Mtangazo

    Biashara ni matangazo hata kama unafanya nje ya mlango wako hakikisha kuwa watu wanajua unachouza

Hatua Za Kuanzisha Biashara Ya Genge

  • Anza na uchunguzi na udadisi wa kila kitu kuanzia soko mpaka changamoto
  • Kisha andaa mpango wa biashara ambao unatoa dira ya biashara nzima kuanzia mwanzo hadi mwisho
  • Halafu fanya usajili wa biashara japokuwa sio lazima sana kama ndio unaanza na huna eneo rasmi
  • Na mwisho maandalizi ya eneo la kuuzia kama utafanya katika eneo moja.

Hitimisho

Biashara hii kama zilivyo biashara nyingine zinahitaji moyo wa dhati , nia na mapenzi bila kusahau kujituma sana na uvumilivu wa hali ya juu

Kumbuka kuna nyakati bidhaa zinaweza kupatikana kwa urahisi na zipo nyakati bidhaa hupotea sokoni

Hivyo bei zinaweza kupanda au kushuka sana ndio maana ni lazima kufanya uchunguzi kabla ya kuanza biashara yoyote .

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Wazo La Biashara Ya Usafi Wa Ofisini6 Min Read

Next Post

Wazo La Biashara Ya Matunda5 Min Read

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.