You Can Win If You Want

Jifunze Kusamehe Hata Kama Hujaombwa Msamaha1 Min Read

Moja kati ya kanuni kubwa zaidi ya kupata amani ya maisha ni kusamehe kwa moyo mmoja

Haijalishi umekosewa kiasi gani huko nyumba, leo au wakati ujao..

Bila kujali maumivu, mateso na hasara ulizopata samehe kwa moyo mmoja

Usiweke vitu moyoni wakati huo huo unateseka kwa mambo ambayo hayana faida tena

Usibebe mzigo wa mateso kwa vitu ambavyo havina maana tena

Usishindwe kusonga mbele kwa sababu ya mambo yasiyo na tija yoyote

Acha maisha mengine yaendelee na fanya kama hakija tokea kitu kabisa

Wakati mwingine mzigo wa kumbu kumbu na visasi Ndio chanzo cha mateso na maumivu kwenye maisha yako

Kukumbatia mambo yaliyopita huweza kuwa chanzo kikubwa cha kikwazo kwenye mafanikio yako

Sio lazima uombwe msahama ndio usamehe, kumbuka sio wote huhesabu kosa palipo na kosa,

Kuna mwingine akikukosea kwake ndio faraja yake ilipo

Kwanini ujiumize kwa sababu ya mtu au watu ambao hawaoni tatizo kwenye tatizo?

SAMEHE, sahau na endelea na maisha yako mengine

Usimchukie mtu kwa sababu zozote zile wala usilipize ubaya wowote

Acha hatma Iamue yenyewe..

Usipoteze muda wako kuweka vitu ambavyo vitakujazia nafasi ya kupokea yaliyo bora zaidi

Makosa ya zamani, ya sasa na hata yajayo hayapaswi kuishi ndani ya akili yako

Tumia muda wako kuanzia sasa kuachilia visasi, chuki na hasira zote ulizonazo na kamwe usiruhusu kubeba chuki zijazo kwenye moyo wako tena.

Samehe, sahau na anza upya maisha yako.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Wazo La Biashara Ya Mahindi Ya Kuchoma4 Min Read

Next Post

Biashara Ya Mahindi Ya Kuchemsha5 Min Read

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Huruhusiwi ku copy. Asante.