You Can Win If You Want

Mbinu Za Kupata Msaada Wa Mtaji

Mbinu za kupata msaada wa mtaji

Msaada wa mtaji unaweza kuwa jambo Rahisi au Gumu kutoka kwa mtu mmoja na mtu mwingine hasa katika Dunia ya sasa

Maisha ya sasa kila mmoja anaangalia maslahi ya upande wake na sio Rahisi kuamini na kumsaidia mtu mwingine Haraka,

Hasa kama hana uhusiano wa moja kwa moja na muombaji, au kama jambo halina manufaa sana kwa upande wake

Lakini pia ugumu huja kutokana na historia za UKOSEFU WA UAMINIFU kwa wanaosaidiwa, Yaani watu wengi wanaoomba msaada huenda kinyume na maubaliano

Hali hii imefanya watoaji wengi kuchoka na kusitisha misaada hasa kwa watu wasio wajua kabisa .

Hivyo basi vijana wengi wamekwama wakiwa na Mawazo mazuri ya Biashara lakini hawana msaada wa mtaji

Kama wewe ni miongoni mwa watu wanaotaka msaada wa mtaji na umetoka katika Familia masikini jua kabisa kuwa unapaswa kuweka jitihada za ziada.

Ikiwa ukoo wako hauna uwezo , namna ya kukupa msaada wala huna kazi ya kukuingizia kipato cha kujitosheleza kutunza pesa,

Unapaswa kujitoa sana bila kuchoka wala kukata tamaa kwa ajili ya kutengeneza maisha yako na kupambania wazo lako.

Maisha Hayana Huruma

Maisha hayana huruma na mtu hata kama una kila sababu za kuhurumiwa!!!

Endapo hutofanya kitu kwa ajili ya maisha yako jua kuwa na maisha hayatofanya kitu kwa ajili yako.

Lazima udhamirie na uache kutia huruma za kwenye maisha na kujiona kama umelaaniwa au umetengwa

Watu hawana muda wala huruma kwa mtu kisa ni masikini ikiwa hawanufaiki kwa chochote kupitia umasikini wako

Kama hutojiinua na kujipambania elewa kuwa hakuna atakae kupambania kamwe , Maisha yako ni jukumu lako mwenyewe

selective focus photographed of green mountain
Photo by Archie Binamira on Pexels.com

Utawezaje Kupata Msaada Wa mtaji Haraka?

Mbinu Ya Kwanza

Kama bado hujapata wazo la Biashara ya kufanya soma hapa ujue njia unazoweza kutumia kupata wazo

Ikiwa una wazo lako na unataka msaada wa mtaji kutoka kwa watu iwe wa karibu yako au wa mbali basi jitahidi kufuata hatua hizi.

Andaa wazo lilochambuliwa

Hakikisha kuwa kitu unachotaka kufanya umekiandaa kwa mfumo wa maandishi yani mpango wa biashara

Pia onesha kwa uwazi kabisa namna ambavyo mtoaji atanufaika na kupata faida kupitia swala lako

Usioneshe kama unataka faida kwanza mpe yeye kipaombele na changanua wazo lako kwa ukweli na mapana

Onesha faida , hasara , changamoto, mtaji husika wote , makadirio ya mauzo kwa miaka angalau 3 ya awali, masoko na mengineyo

Usioneshe uongo wa aina yoyote kuwa mkweli na jiamini kwa nguvu zako zote.

Fanya Uchunguzi Wa Watu Au Taasisi Zinazoweza Kukusaidia

Huwezi kuomba msaada kwa watu usiowajua yani lazima ujue unaanzia wapi na kumalizia wapi

Na kabla hujasema watu hawana msada hakikisha kuwa umechunguza ndege wako kabla hujarusha manati yako

Sio kila mtu utakae kutana nae anaweza kukupa msaada kwahio chunguza kwanza uwezo wa mtu, Imani yake , Huruma , Uhitaji wake na hata historia yake ya utoaji

Pia lazima uchunguze kiwango cha uchumi wa mtu kama kinakidhi kukusaidia maana sio kila mtu anaweza kupunguza bajeti yake

Kumbuka Uwekezaji kuna kupata na kukosa sasa Mtu hawezi kutoa kitu chake cha mwisho ikiwa anajua anaweza akapata hasara

Ila ukipata mtu mwenye uwezo mkubwa angalau jambo halitokuwa na ugumu sana.

Orodhesha Watu Wote Wanaoweza Kukusaidia Au Taasisi Za Misaada

Hapa usiogope weka Idadi kubwa kadiri utakavyoweza, andika ila anaekujia kichwani iwe anakujua au hakujui kabisa

Angalia watu wenye uwezo kiuchumi angalau wanaoweza kukupa kiasi unachotaka bila kutumia nguvu sana

Usidharau mtu lakini angalia ambae angalau una uhakika na uchumi wake

Anza ngazi ya Familia yao , Marafiki, Mtaani, Kata , Wilaya, Mkoa na hata Nchi nzima au nje ya nje kupitia watu au Taasisi

Wanaweza kuwa viongozi , Walimu wako wa sasa au waliopita, Marafiki zako, Mjirani zako, au mtu yoyote unaemjua hata kama hakujui

Usiogope muonekano wa nje wa mtu hata kama anaonekana mgumu kuingilika wewe andika kila mmoja kwa namna yake

Andika majina na namna ya kumpata iwe ana kwa ana , namba ya simu,akaunti za mitandao ya kijamii na hata Email kulingana na ukaribu wako wa kumfikia kirahisi.

Weka Nia Na Dhamira Ya Dhati Kutoka Moyoni

Siku zote penye nia pana njia na hakuna kinachoshindikana chini ya jua hata kama kitachelewa

Tia nia ya dhati kabisa na dhamiria kuwa hutokubali mpaka ufanikiwe, kumbuka sio rahisi kupata pesa ya mtu kwa urahisi

Jitihada , ubunifu na uvumilivu unahitajika sana kuweza kufanikisha, hivyo bila nia na dhamira ya dhati utashindwa kutimiza lengo lako.

Anza Na Watu Wa Karibu Kufikika

Hasa wale ambao umewazoea sana au angalau wanakujua, hawa ni kama ndugu , marafiki , viongozi wako wa ibada , mtaani na hata walimu wanao kufahamu vizuri

Kisha kama lengo litakuwa bado utafuata wale ambao unawajua ila wao hawakujui kuanzia ngazi ya mtaa wako na kuendelea

Usianze na watu wa mbali sana ikiwa watu wa karibu yako wapo kisa aibu au uoga kumbuka maisha hayataki UOGA.

Tumia Njia Sahihi Ya Kumfikia

Njia ya ana kwa ana ndio njia sahihi zaidi na njia bora ya kuomba msaada wa mtaji au msaada mwingine wowote

Ni mara chache sana mtu kukukatalia jambo ikiwa umeonana nae macho kwa macho na kumueleza shida kwa kinywa chako

Lakini kama njia hii haiwezekani kutokana na Ratiba ya mtu , uzito wa kumfikia na hata umbali basi tumia nji ya Kumpgia simu, kutuma ujumbe au Email

Na kama huna vyote basi Muandikie kupitia kurasa wake wa mtandao wa kijamii anaotumia.

Vaa Vazi La Uhitaji

Epuka kuto kujitosheleza kiuhitaji, yaani kama kweli una nia na uhitaji wa dhati lazima utajionesha tu machoni au hata kwenye maandishi yako

Mtu anaetaka msaada wa kweli hujulikana na ambae hana nia pia huonekana kwa macho rahisi sana

Hivyo kuweza kushinda moyo wa mtu haraka lazima uwe na vazi la uhitaji rohoni na ndani ya moyo wako wote.

Vazi la uhitaji hujionesha machoni kupitia mambo haya

  • Namna unavyoongea
  • Unyenyekevu wako
  • Jinsi unavyosisitiza
  • vile unavyo jiamini
  • Uvumilivu, usikivu na umakini wa ufatiliaji
  • Namna ulivyo na jitihada na kutoonesha hali ya kukata tamaa nk.

Anza Kumkabili Mmoja Mmoja

Usiwe na haraka sana jitahidi kuanza na mmoja baada ya mwingine nenda na mpango wako wa Biashara mkononi lakini usiuoneshe kwanza

Ikiwa ni maongezi ya ana kwa ana ongea kwa mdomo kwanza Jieleze kwa kujiamini na Usioneshe hali ya hofu

Hakuna Binaadamu tofauti na mwingine yani wote tupo sawa tumezidiana Umri, vyeo na uchumi tu

Hivyo si sahihi kumuogopa mtu yoyote kupindukia bali jenga heshima pekee.

Akivutiwa na wazo lako basi Muachie mpango wako wa Biashara wa maandishi kisha subiri jibu lake

Endapo ni kwa njia ya simu anza maongezi kwanza kisha akiomba mpango wa Biashara ndio mtumie baadae

Na kama ni kwa njia ya Email ,sms au akaunti za mitandaoni anza kujitambulisha kisha Eleza shida yako kwa ufupi na subiri jibu lake

Ikiwa haitojibiwa mkumbushe mara tatu katika vipindi tofauti kisha tuma mpango wa Biashara yako moja kwa moja.

Watu wengi wana pesa na hutafuta mahala pa kuziwekeza ziweze kuzalisha kwahio usiogope kwamwe kuomba msaada.

seaside
Photo by Fabian Wiktor on Pexels.com
Mbinu Ya Pili

Oesha uwezo wako kwanza

Hapa ili kupata msaada wa mtaji anza kwanza na ulichonacho kupitia uwezo wako binafsi wewe mwenyewe kwanza

Kama hujajua namna ya kuanza Biashara bila mtaji au kwa mtaji mdogo ulionao na kupata mafanikio basi soma hapa

Ni rahisi sana kupewa msaada ikiwa utaonekana kwa macho jitihada zako za kila siku , watu hawapendi kupoteza pesa zao

Na hakuna mtu ambae atafurahia kuona anapata hasara au kuamini kitu ambacho hakipo mbele yake

Ila ni rahisi sana kwa watu kuongezea kile wanachokiona kimeanza hata kama kina uchache ndani yake

Hivyo lazima uoneshe kwa vitendo kwanza uwezo wako kisha ufanye wengine wakupe sapoti unayotaka

Anza na ulichonacho , anzia ulipo na tumia vile vilivyo ndani ya uwezo wako kwanza onesha nia jitihada na dhamira ya dhati

Kisha itakupa urahisi wa kushawishi wengine kukusaidia na kuonesha sapoti zao na hata wasipokusaidia utapata namna ya kusimama imara mbeleni

UKITAKA LIFTI YA KWENDA KIGOMA HUWEZI KUIPATA UKIWA CHUMBANI KWAKO; NI LAZIMA USOGEE ULIPO USAFIRI WA KWENDA KIGOMA.

Chukulia mfano unataka kwenda mahala popote lakini huna nauli ya kukufikisha uendapo , sasa kukaa chumbani kwako na,

Kulia sana au kumuomba Mungu ukiwa ndani hakutoweza kufanya muujiza wowote wa safari ya usafiri kuja kukufuata!

Jisaidie Wewe Kwanza

Hata Mungu anataka kwanza UJISAIDIE KISHA NAE AKUSAIDIE yaani hakuna mahala utafika kwa kulala ndani kisa huna nauli

Wala hakuna usafiri utashuka kutoka ndani ya machozi yako wala Nyumba ya ibada unakokesha kuomba Dua bila kuchukua hatua.

Ila ukiinuka na kuanza kutembea mpaka zilipo gari au usafiri wa mahala unataka kwenda basi kuna uwezekano mkubwa wa kupata msaada

Inuka tembea kwa mguu taratibu kufuata njia ya sehemu unakoenda huku ukisimamisha usafiri kwa hisia na sura ya uhitaji

Au fika zilipo gari husika na anza kuomba wahusika au wanaokuzunguka ukiwa hapo hapo mbele ya usafiri

Huku ukiwaelezea wanao husika sababu ya msingi kwanini wakupe lifi?

Ukifanya hivyo nina amini kuwa Lazima utapata msaada au hata utapewa njia ya rahisi ya kufika uendako kwa msaada mwingine

Na hata ukikosa kabisa basi utakuwa umejifunza kitu katika hilo na itakujengea uzoefu wa nini chakufanya wakati mwingine,

Hii ni tofauti kabisa na kama ungekaa ndani tu bila kufanya chochote kwa kusubiria miujiza au kulia sana na kuhisi umepungukiwa

Anza kuonesha uhitaji kwa vitendo kisha utapata msaada unaotaka au njia sahihi ya kukufikisha uendeko

Hata Mungu ni rahisi sana kukusogezea msaada baada ya kuona nia yako kupitia vitendo unavyofanya

Mguu Uliotoka Mtume Kauombea

Hii ni Imani ya Waumini wa Dini ya Kiislamu , yaani ina maana kuwa ukitoka ndani ya nyumba yako na kwenda kujitafutia Riziki yako,

Tayari unakuwa na baraka za Mungu kupitia Mtume wake na Mungu atakusaidia katika jitihada zako.

Hivyo basi tukirudi katika uhalisia wa mada hii ni kuwa ili kupata msaada wa mtaji anza na kidogo ulichonacho

Kipende na kitumikie kwa jitihada zako zote huku ukiendelea kutafuta watu wa kukusaidia mbeleni

Kuna uwezekano mkubwa hata wakaja wenyewe kukusaidia bila wewe kuwatafuta kumbuka watu wana pesa na wanatafuta pakuziweka ziwazalishie

Mbinu Ya Tatu

Saidia Wengine Na Wao Wakusaidie

Kumbuka msemo wa kiswahili kuwa MKONO MTUPU HAULAMBWI maana yake ni kuwa watu watakusaidia ikiwa na wao umewasaidia

Hakuna mtu ambae hataki msaada hata kama ana mafanikio makubwa unavyodhani, kila mmoja hutamani kupata msaada kutoka kwa wengine

Sio lazima msaada uwe pesa bali hata mawazo na mambo madogo madogo au hata zawadi ndogo inayoonesha upendo na thamani ya mtu

Usipende kupokea tu au kutaka kusaidiwa huku ukiwa na mkono wa birika yani chako chako na cha wenzio pia chako!

Tafuta namna ya kumsaidia mlengwa wako kwanza unaetaka msaada kutoka kwakwe katika namna yoyote rahisi kwako

Unaweza kumpa mbinu au ushauri wa kufanya jambo lake vizuri au kujisogeza karibu pia Kumsaidia mambo madogo madogo

Hata majukumu yake ya kazi , nyumbani na popote pale ili aone faida na thamani yako kwanza kabla hujaanza kuomba msaada .

Toa ili upewe zaidi toa muda wako, nguvu zako ,maarifa yako na hata zawadi ndogo ndogo kwa ufupi ni kuwa JIPENDEKEZE UNAPOWEZA.

Mambo Ya Kuzingatia Unapoomba Msaada Wa Mtaji

  • Epuka kuomba msaada kupitia kurasa za mitandaoni
  • Epuka kulazimisha sana kusaidiwa kutoka kwa mtu mmoja
  • Kataa roho ya kukata tamaa na kuchoka
  • Usiombe vitu visivyo na tija
  • Usimchukie aliyekataa kukusaidia sio laizima kukubaliwa ombi na anaweza kukusaidia wakati mwingine
  • Usiamuamini aliyesema atakusaidia kwa maneno matupu.

Hitimisho

Kwenye haya maisha usitegemee bahati nasibu ikufuate , inuka na pambania bahati yako kwa kuivuta ije kwako kwa vitendo

Usingoje msaada ukufuate ulipo simama na pambania msaada unaotaka kwa vitendo

HAKUNA KITU KINACHOTOKEA KWA BAHATI MBAYA TENGENEZA MAZINGIRA ILI VITU VITOKEE.

#REMEMBER YOU CAN WIN IF YOU WANT (UNAWEZA KUSHINDA IKIWA UNATAKA)

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Namna Ya Kuanza Biashara Bila Mtaji

Next Post

Mbinu Za Kupata Mtaji Wa Kuanza Biashara

Comments 1

Acha Comment Yako

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.