You Can Win If You Want

Namna Rahisi Ya Kupata Mtaji Wa Biashara Kwa Wenye Kipato Kidogo5 Min Read

Namna ya kupata mtaji

Utangulizi

Mtaji wa biashara ni changamoto inayosumbua watu wengi sana hasa wenye kipato kidogo na wasio na kipato cha uhakika

Hali ambayo imepelekea watu wengi sana kukwama kwenye utekelezaji wa mawazo na ndoto walizonazo kwenye maisha

Wengi wanatamani sana kujiajiri na kuwa na maisha ya uhuru kupitia biashara zao binafsi wanazotaka

Na asilimia kubwa wamechoka maisha ya kuajiriwa ila hawana jinsi ya kuacha kazi kwa sababu ya ukosefu wa mitaji

Jambohili pia linagusa vijana wengi ambao wamemaliza masomo yao na kukosa ajira rasmi au kukosa ajira kabisa

Wanatamani kugeukia suala la kujiajiri kama wanavyo sisitizwa na mamlaka mbali mbali ila changamoto mtaji!

Sasa wengi sana hujikuta wakipoteza muda na miaka mingi kungoja miujiza ya kupata mitaji kitu ambacho hufifiza matarajio

Hakuna namna ya kupata mtaji hasa kwa watu wanaotoka katika familia masikini na zenye kipato cha chini

Bila kusahau hao waajiriwa rasmi ,uzito wa majukumu na changamoto za maisha zinakwamisha ndoto zao

Kujiajiri sio jambo rahisi wala gumu sana bali ugumu na urahisi wakati mwingine huchangiwa na kipato.

mtaji wa biashara
Photo by Photo By: Kaboompics.com on Pexels.com

Mtaji Wa Biashara Ni Nini ?

Mtaji wa biashara ni kitu chochote kinachoweza kutumika katika uanzishaji au uendelezaji wa biashara ya aina fulani

Sio lazima iwe pesa peke yake bali vitu vingine vyote ambavyo hutumika kusaidia biashara kufanyika

Kwa maana kuwa unaweza kuwa na pesa kamili ya kununulia vitu au ukawa na vitu hata kama ni vitu vya zamani

Wengi wamezoea kuwa mtaji ni pesa taslimu ambayo ndio haswa huhitajika kuweza kuanza biashara

Wanasahau kabisa kuwa kuna vitu vingi pengine hata wanavyo na wanavimiliki pia ni mtaji wa biashara kulingana na wazo

Hivyo basi linapokuja suala la mtaji wa biashara lazima liambatane na aina ya biashara inayohitajika

Kisha orodha kamili ya vitu vyote vinavyotakiwa na baadae ndio itafahamika kuwa vitu vipo au vinahitaji kununuliwa.

Kwahio mtaji ni zaidi ya pesa taslimu kutegemea na aina ya biashara inayotaka kuanzishwa!

Vile vile zipo biashara ambazo zinaweza kuanzishwa bila mtaji kabisa ,kwa mtaji mdogo sana na mkubwa.

Mbinu Ya Kupata Mtaji Wa Biashara Kwa Wenye Kipato Kidogo

Mbinu hii inaweza kutumiwa na mtu yoyote ambae amekwama kupata mtaji wa kuanza biashara

Iwe kwa sababu za kipato au sababu za ukosefu wa pesa ya pamoja kuanza biashara

Mbinu yenyewe kubwa zaidi ambayo hurahisisha ukusanyaji wa mtaji ni (kuwekeza kidogo kidogo)

Baada ya kuwa na wazo la biashara unayotaka kufanya kisha kujihakikishia kwa dhati kuwa ndio kitu unachotaka

Sasa jambo muhimu ni kufanya uwekezaji mdogo mdogo kwenye mtaji unaotaka kuanza nao kwa mara ya kwanza

Utapaswa kununua vitu kidogo kidogo na kutunza ndani kwako hususani vile vitu muhimu zaidi na visivyo haribika

Nunua vitu vyako taratibu bila kuwa na presha kubwa wala wasiwasi sana wa lini utakamilisha manunuzi

Ikiwa kipato chako ni kidogo na huenda unabakiwa na pesa kidogo zaidi basi usiweke ndani pesa

Nenda haraka kanunue vitu unavyotaka kuanzia biashara na tunza ndani kwako.

Wekeza Dukani

Wafanya biashara wengi madukani wanaruhusu mteja kuwekeza pesa kidogo kidogo kama hawana pesa keshi

Hivyo ni rahisi sana kuanza kununua vitu kwa kuwekeza dukani taratibu mpaka pale mtaji utakapo kamilika

Unaweza kununua kitu kimoja kimoja kwa mara moja na kutunza ndani ikiwa unabaki na pesa za ziada

Au kama pesa hubaki chache sana na haitoshi kununua kitu kimoja hata kwa mara moja basi WEKEZA DUKANI.

Tafuta duka la karibu ambalo unalifahamu wanapouza kitu unachotaka kisha ongea na muuzaji

Akupe utaratibu wa kuwa unapeleka pesa kidogo kidogo mpaka pale itakapotosheleza ununuzi wa kitu

Huku anakuandikia risiti ya ushahidi wako kila unapopeleka pesa bila kusahau saini na tarehe za kumbukumbu

Kila unapokamilisha chukua kitu chako na tunza ndani kisha endelea na utaratibu huohuo mpaka utakapo kamilisha vyote

Utashangaa haitochukua muda mrefu utakuwa umekamilisha mahitaji yote unayotaka bila kutegemea.

Mara nyingi utaratibu huu ,huleta msukumo na shauku ya kukamilisha vitu vyako kila saa

Shauku hujenga hali ya kuzuia matumizi yasiyo ya lazima na hufungua akili kutafuta pesa za ziada

Ni tofauti na kukaa kusubiri upate pesa ya pamoja ,hujenga uvivu wa kufikiri na matumizi mabaya zaidi

Hivyo basi njia ya uwekezaji ni njia rahisi ya kupata mtaji wa biashara hasa kwa wale wenye kipato kidogo.

Njia hii ni rahisi na salama zaidi kuliko kutunza pesa ndani au kucheza michezo na upatu.

Hatua Za Kuwekeza Mtaji Wa Biashara

  1. Jua aina ya biashara unayotaka kufanya

    Huwezi kuanza kufikiria mtaji kama hujajua hasa kipi unataka kufanya kwa kutumia huo mtaji hata kama bado huna pesa

  2. Fanya uchunguzi

    Chunguza kila kitu unachopaswa kujua kuhusu hio biashara unayotaka kwa undani ili uwe na taarifa sahihi

  3. Andaa mpango wa biashara na ainisha mahitaji ya msingi

    Wakati unaandaa mpango wa biashara zingatia kipengele cha mtaji na vitu vyote unavyotaka kuwa navyo ili biashara yako ianze usiache hata kimoja iwe kikubwa au kidogo

  4. Anza na vitu vya muhimu

    Angalia vitu ambavyo ni muhimu zaidi kuliko vyote kwanza kwenye hio biashara ili ianze kufanyika ndio uanze navyo

  5. Tafuta duka la karibu

    Duka ambalo wanauza hiko kitu au vitu unavyotaka kisha ongea na muuzaji ili uwe unapeleka pesa kidogo kidogo na baada ya kukamilisha akupe kitu chako

  6. Panga bajeti rasmi

    Kupitia kipato chako unachopata tenga matumizi yako na yapunguze zaidi ili uweze kubaki na pesa ya kuwekeza

  7. Anza kwa vitendo na chukua hatua

    Baada ya kujiridhisha sasa anza mara moja uwekezaji wako haijalishi hata iwe elfu 5 au elfu 10 peleka dukani ukimaliza chukua kitu weka ndani

  8. Rudia mchakato

    Kwa vitu vyote rudia mpaka ukamilishe mahitaji yote unayotaka

Hitimisho Na Mambo Ya Kuzingatia Unapowekeza Mtaji Kidogo Kidogo

Hata kama una kipato kidogo, huwa kuna tabia ambazo hupelekea chanzo cha kumaliza pesa za akiba mara kwa mara

Bila kusahau changamoto za maisha za hapa na pale huchangia sana pesa kutumika nje ya malengo muhimu

Kwahio kutunza pesa ndani sio njia sahihi sana kama unataka kupata mtaji haraka ni bora uwekezaji wa manunuzi

Ikiwa utafanya utaratibu huu ni jambo zuri sana japo linaweza kuwa na changamoto kadhaa ambazo hutokea

Ila kitu cha msingi ni kuwa makini na kuzingatia vitu muhimu ili kufanikisha jambo lako kwa kuzingatia:

  • Duka la mtu muaminifu
  • Risiti ya malipo
  • Kwenda mara kwa mara kupeleka pesa
  • Usalama wa mahala utakapotunza vitu vyako.
Share this article
Shareable URL
Prev Post

Namna Ya Kufanya Maamuzi Sahihi7 Min Read

Next Post

Mbinu Za Kuishi Na Watu Vizuri6 Min Read

Comments 25
  1. Laptop yangu nimenunua kwa system hii ya kulipia kidogo kidogo, highly recommend it kama una kipato kidogo au ni mwanachuo

  2. Mimi changamoto niliyonayo ni ya kupata wazo la biashara nzuri. Yaani utakuta nafanya research weeh, kila kitu unakuoa unaona kama kinalipa mara unakutana na simulizi za wengine kua hio biashara haifaii yaani nabaki nimeganda tu

    1. Pole sana kwa changamoto, unapotaka kuanza kitu usiangalie wengine utakwama, jangalie ww na moyo wako lakini pia pitia baadhi ya makala za biashara hapa hapa zipo zimeandaliwa chagua unayotaka na anza kufanya

  3. Andiko zuri sana hili, limenikumbusha enzi izo nimeamua kujilipua kuanza biashara ya kuuza uji. Hakika maisha ni fumbo kubwa . Be blessed 🙏

  4. Natamani kuanzisha salon ya kwangu siku moja, ngoja niendelee kujichanga. Nimepata motisha mpya

  5. Samahani dada, je njia hizi naweza zitumia kama kitu ninachotaka kufanya ni cha mtandaoni?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.