You Can Win If You Want

Namna ya kujiajiri baada ya kumaliza chuo kupitia taaluma yako

Kujiajiri kupitia taaluma yako ni kitu  cha msingi na kitu kinachowatesa watu wengi sana kwani wanamaliza masomo wakiwa na matumaini ya ajira

Duniani changamoto ya ajira limekuwa tatizo kubwa sana , japokuwa kuna baadhi ya nchi angalau kuna unafuu wa upatikanaji ajira, suluhisho ni kujiajiri kupitia taaluma yako

Tanzania ni moja kati ya nchi zenye uhaba mkubwa wa ajira serikalini na sekta binafsi,

kuna baadhi ya vigezo nje ya taaluma yako kama ukivikosa basi sahau kabisa kitu kinaitwa ajira.

Kujiajiri kupitia taaluma
  • Mfano Konekshi ya watu mbalimbali mbali hasa viongozi, nimeshuhudia watu wengi ambao hawana GPA kubwa wakiajiriwa kwakua tu wana ndugu zao katika uongozi wa juu
  • Rushwa hasa ya pesa, maana Rushwa ya ngono kwa maisha ya sasa ni kama haina nguvu kubwa sana hivo usijisumbue hata kuwaza kutoa ngono upate kazi na pia kama Huna pesa za kuhonga nyingi sahau ajira na wakati mwingine unaweza kutoa pesa na usipate ajira

Inaumiza sana kuteseka zaidi ya miaka 16 kusoma, umepoteza muda mwingi na pesa nyingi

Halafu unahitimu unakosa ajira, hakuna namna zaidi ya kujiajiri kupitia taaluma yako tu

Lakini pia ukosefu wa ajira umesababishwa na mambo mengine  kama vile

  • Kuongeza kwa idadi ya wahitimu na kusababishia ushindani mkubwa katika soko la ajira , miaka ya nyuma wahitimu wa fani mbalimbali walikuwa wachache sana hivo nafasi za ajira zilihitaji watu wengi lakini sasa idadi ni kubwa kuliko hata uhitaji wa ajira zenyewe
  • Ukosefu wa viongozi yenye weledi na ubinafsi wa viongozi hivyo kupelekea hata maeneo yanayohitaji wataalamu kushindwa kufikisha kwasababu ya weledi wa kazi na matumizi ya mabaya ya pesa za umma, kuna shule nyingi zina uhaba wa walimu na walimu waliohitimu wapo wengi mtaani lakini serikali inasema haina pesa za kutosha! Ila wanazidi kujilimbikizia Mali

Hivyo ukiwa kijana ambae umemaliza chuo, mtoto wa masikini,

Huna yoyote unaemjua kwenye uongozi wa juu na Huna muelekeo wala uhakika wa ajira

usipoteze muda wako mwingi kuhangaika na utafutaji wa ajira! Jiajiri kupitia taaluma yako

Tafuta ajira huku unajiajiri

Sisemi usitafute ajira ya ndoto zako lakini najaribu kukuepusha na upotezaji muda na majuto baadae

Kutumia miaka 3 au 5 kutafuta ajira huku ukiwa huna uhakika wa maisha yako ya mbele

Naona kama sio kitu chenye afya sana, ukizingatia umri haurudi nyuma

Hivyo tenga muda wako vizuri ikiwezekana hata kabla hujatoka chuoni “jua nini unataka kufanya mtaani nje ya ajira rasmi “

Yani lazima uwe na wazo la kukuingizia pesa iwe utaajiriwa au hutoajiriwa Ila ndani ya taaluma yako

Na wazo litafute ukiwa bado chuoni na endapo umeshahitimu basi anza muda huu

Waza kitu cha kufanya nje ya ajira kupitia taaluma uliyosomea na elimu uliyoipata

Mtaani kuna pesa nyingi sana tafuta nyavu yako na uzitege!

Mimi ninaamini kuwa  nchi kama Tanzania fursa bado nyingi na kila mmoja anauwezo wa kuchukua fursa yake na akaingiza pesa nyingi kikubwa ni DHAMIRA NA IMANI

Mfano umesoma sheria jiulize hapo mtaani  unapokaa raia wangapi wanajua haki zao! Utagundua hakuna na kama wapo haizidi asilimia 1%!

Sasa jiulize kuna wanasheria wangapi wanahitimu kila mwaka vyuoni lakini hakuna mafanikio ya moja kwa moja kupitia Elimu zao kwa jamii?

Haya na wewe leo hii umemaliza sheria Ila unangoja kuwa wakili wa serikali! Kuna mahakama ngapi hapa Tanzania?

Zipo sekta binafsi ngapi hapa Tanzania? Na kuna wahitimu wangapi wanaziangalia hizo sekta na mahakama!

Huna pesa mfukoni Ila una elimu ya sheria!  Huna pesa Ila una wateja ambao Ndio hao hao raia wa mtaani wamejaa wengi sana

Sasa badala ya kusubiri ajira kwanini usitumie Elimu yako kupata pesa? Biashara sio mtaji

Chagua kipengele kimoja tu chenye uhitaji mkubwa labda ndoa, fundisha kina mama na kina baba sheria za ndoa,

Au sheria za mirathi (watu wana kufa kila siku), sijui sheria za kazi nk

Jiulize kuna single mother wangapi wanatesa na watoto kwa kutojua tu sheria  na haki zao kwa wazazi wenzao?

Kuna wa mama wangapi wanateseka na ndoa kwa kutojua tu sheria za ndoa na haki zao?

Kuna wafanyakazi wangapi iwe viwandani au sekta ndogo ndogo wanateseka kwa kutojua haki zao?

Tatua changamoto za jamii moja kwa moja kwa kupitia taaluma yako

Hebu mimi na wewe tujiulize kuna migogoro mingapi ya ardhi kila kukicha! Watu hawajui  hatua za kufuata kununua na kulinda ardhi zao!

Lakini wasomi na wataalamu wa ardhi wapo mtaani wanangoja ajira za serikalini

Chagua eneo moja tu ulilosomea na unaloliweza sana kisha jifunze mbinu za kuuza (sales)  kupitia vitabu kama sales like crazy uteke wateja

Pia  kuna channel kama YouTube kuna video nyingi zina fundisha mbinu za kuuza na kupata wateja

Kwa kuanza anza mtaani kwako, tumia simu yako, na usifirikie faida kwanza

Ila jenga uaminifu na fanya watu waone faida ya unachowasaidia

Umesoma sijui human rights au human  resources? Itumie mtaani kwako! Saidia watu wako kwanza wakati unasubiri hizo ajira hewa!

Umesoma Accountant, au labda economics, sijui marketing kwanini sasa huitumii mtanii kwenu?

Kuna wafanya biashara wangapi wanafanya biashara kimazoea hapo mtaani kwenu na hawajui wafanye nini kwenye mambo ya fedha!

Hawajui wafanye nini kukuza biashara zao wala hawana uelewa na mambo yote ya biashara

Nachojua wapo wengi tu na wana pesa ndogo ndogo za kuweza kukulipa kama tu utajua namna ya Kuwasiadia na wakafanikiwa 

Umesoma agriculture, kijijini kwenu kuna mashamba kibao yanahitaji wataalamu wa kuelekeza watu wapate faida katika kilimo na ufugaji!

Basi nenda kijiji kingine kama unaona aibu kuonekana msomi halafu upo mashambani

Fikiria wazo ndani ya taaluma yako

Umesoma social development, ehe una project gani ya kuleta maendeleo katika jamii yako? Au unangoja kuwa afisa mtendaji!

Sawa una haki ya kuwa afisa mtendaji lakini jiulize kuna wahitimu wangapi wa social works na kuna idadi ya kata ngapi zinahitaji afisa watendaji!?

Kila mwaka kuna wahitimu wengi wa social development lakini, 

Tanzania bado  masikini vile vile hakuna hata project kubwa ya kuondoa au kupunguza umasikini

Umesoma Ualimu iwe wa sekondari au msingi na upo mtaani hapo, angalia idadi ya watoto wanao soma kisha jiulize wana uhitaji gani kupitia taaluma yako?

Hakuna mzazi asiyetaka mwanae afaulu anza na mtoto mmoja ambae ana nia ya kusoma

Mfundishe somo unaloliweza sana kwa muda wako wa ziada hata nusu saa tu hapo hapo nje ya unapokaa  na usiombe pesa!

Ukifundisha vizuri ndani ya mwezi atawaambia wenzake  na idadi itaongezeka,

Taarifa zitafika kwa wazazi hapo sasa Ndio weka mikakati ya malipo kwa kuangalia uwezo wao

Heshimu muda na gharama ulizotumia kupata taaluma yako usikubali kujitolea!

Fikiria miaka zaidi ya 16 umepoteza vitu vingi, ulivumilia mambo mengi na hata wazazi walijinyima kwa ajili yako

Halafu leo hii unaenda kujitolea miaka zaidi ya mitatu kwenye taasisi ya mtu halafu muda wa kuajiri ukifika wanaleta watu wao!

Kuna faida za kujitolea  sikatai lakini fikiria umejitolea miaka 3, hulipwi au unalipiwa pesa kidogo sana

Ambayo haitoshi hata nauli  halafu muda unafika wa kuajiriwa analetwa mtu mwingine!

Hebu hata wewe waza tu je ungetumia hio miaka 3 kujiajiri kwa wazo lako ndani ya taaluma yako ungekuwa na wateja wangapi?

Hata kama unaamini katika kujitolea basi angalau panga muda wako vizuri fanya vyote

Yani jitolee kwenye hio taasisi na jitolee kwenye biashara yako

Huwa nina shangaa sana mtu anapoteza muda wake mwingi kujitolea kwenye biashara au taasisi za watu wengine

Bila hata malipo ila hachoki na hakati tamaa lakini anaona ugumu kujitolea kukuza wazo lake!

Mtu anafanya sales kwenye kampuni za watu na anaingiza wateja wengi ila anaona shida kutafuta wateja wake hata kwa mara moja moja! 

Tumia mitandao kujiajiri kupitia taaluma yako

Kama unaona aibu kuonekana msomi mshamba hapo mtaani au kijijini kwenu basi mitandao naamini ni sehemu sahihi zaidi

Huo muda unaotumia kuperuzi na kufatilia maisha ya wengine hebu badilika na tumia kupost taaluma yako.

Jiweke kisomi, na ongelea huduma zako kwa njia ya kuelimisha kupitia Facebook, Instagram , jamiiforums nk

Elekeza watu kile unachokijua iwe sheria, uhasibu, uchumi, siasa, Ualimu nk

Mtaji ni muda wako kidogo, simu na vocha tu, naamini ukiwa na nia na dhamira

Ndani ya miezi michache utapata watu wa kuwahudumia, kikubwa usiweke tamaa mbele anza na kujitolea!

Heshimu taaluma yako na usifanye biashara (kazi) nje ya taaluma yako

Mfano umesoma sheria halafu unauza maandazi, umesoma Ualimu unaamua kuuza mitumba

Umesoma agriculture unaenda kubeba zege, umesoma maendeleo ya jamii tunakukuta unauza duka la nguo za watoto, mesoma economics unaenda kudanga!

Umesoma sijui project planning halafu unakuja kuuza mgahawa!

Sasa aliyesoma hotel management afanye nini? Au yule mama asiye na elimu kabisa mtaani afanye nini?

Haya mambo Ndio yameshusha thamani ya elimu ya Tanzania na mpaka sasa msomi anadharaulika mitaani

Haiwezekani msomi awaze Sawa na yule ambae hakusoma

Fanya hizo kazi lakini kwa muda ambao unajitafuta huku unajitolea kupitia taaluma yako halisi

Na kama umeamua kufanya hizo biashara, 

Inawezekana ulitamani kuwa hivyo toka awali sasa kwanini ulipoteza muda na pesa kusoma kitu ambacho hukipendi na ulijua hutokitumia!

Jiajiri kupitia taaluma kuipa hadhi jamii na kurudisha thamani ya elimu yako

Naomba nisieleweke vibaya, sipingi wala kudharau maoni na maamuzi ya mtu,

Sikatai kuwa kujitolea kuna faida, sibishi wala kukinzana na yoyote anaejitafuta kwa kufanya chochote

Ila najaribu kuonesha njia kwa wale waliokwama namna ya kufanya maamuzi baada ya Kuhitimu Elimu zao

Hivyo simama katika unacho kiamini maana maisha ni zawadi ya muda mfupi na kila mmoja anapaswa kufurahia kwa namna yake

Kujiajiri bila pesa sio rahisi lakini inawezekana hivyo amua sasa kufanya mabadiliko katika maisha na jamii yako kupitia taaluma yako

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Njia rahisi ya kujitafuta na kujipata

Next Post

Dawa ya msongo wa mawazo

Comments 1

Acha Comment Yako

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.