You Can Win If You Want

Namna Ya Kupanga Malengo Ya Biashara5 Min Read

Utangulizi

Malengo ya biashara ni malengo yanayo tarajiwa kutimizwa katika kipindi fulani cha muda kwenye biashara fulani

Vile vile malengo haya huwekwa na mfanya biashara kwenye biashara yake ili kupata dira kamili ya biashara anayofanya

Malengo ni muhimu sana kwa mfanya biashara yoyote haijalishi ni biashara kubwa au ndogo bila kujali mtaji pia

Yaani ni kama yalivyo malengo ya maisha kwa mtu mmoja mmoja na haya pia hupaswa kupewa kipao mbele kwenye biashara

Ni muhimu sana kuwa na malengo kwenye biashara unayofanya bila kujali aina ya biashara wala mtaji ulionao

Tena hupaswa kupangwa hata kabla hujaanza kabisa biashara yako au wakati unaandaa mpango wa biashara

Japokuwa malengo haya huweza kubadilika kulingana na sababu kadha wa kadha wakati wa uendeshaji,

Lakini dira nzima ya malengo hutoa muongozo na kuonesha njia kwa mfanya biashara kwenye biashara yake

Sababu kubwa zaidi ya kuweka malengo ni kuongeza mzunguko wa pesa faida na kuipa biashara uhai.

malengo ya biashara
Photo by Viridiana Rivera on Pexels.com

Aina Za Malengo

Kama ilivyo kwenye malengo ya mtu binafsi au yale ya maisha pia malengo haya yamegawanyika katika aina 2

  • Malengo ya muda mfupi
  • Malengo ya muda mrefu

Malengo ya muda mfupi

Haya ni malengo ambayo yamepangwa kutimizwa katika kipindi kifupi cha muda kwenye biashara

Malengo haya yanaweza kutoka katika malengo ya muda mrefu lakini yaliyo vunjwa vunjwa ili kurahisha utekelazaji

Kwa mfano kama lengo la biashara ni kuwa na faida ya milioni kumi ndani ya miaka 10 maana yake

Ile mipango midogo midogo na mikakati ya kila siku kuhakikisha lengo la kupata milioni kumi linatimia,

Ndio tunaweza kuyaweka katika malengo ya muda mfupi katika biashara.

Malengo Ya Muda Mrefu

Haya ni yale malengo ambayo huwekwa kwenye biashara kwa kuzingatia kipindi kirefu cha muda

Mara nyingi malengo haya huhusisha picha nzima ya biashara au hata maono mazima ya biashara husika

Malengo haya ndio roho na kiini cha biashara nzima na yaliyo beba picha halisi ya mfanya biashara

Hivyo haya sasa ndio hupelekea kuwepo kwa yale malengo ya muda mfupi ndani ya biashara fulani kwa muda fulani

Mfano wa malengo ya muda mrefu inaweza kuwa kufungua tawi lingine la biashara ndani ya miaka 3 ijayo

Au kusambaza kilo 1000 kila siku za mchele ndani na nje ya Tanzania katika kipindi cha miaka 20 ijayo

Na hata malengo mengine yoyote yale kulingana na mipango ya wahusika binafsi wa biashara hio

Kwahio ile mikakati ya utekelezaji wa lengo kila siku au ndani ya miezi kadhaa ndio huwa malengo ya muda mfupi.

Faida Za Malengo

Kama tulivyoona hapo mwanzo kuwa sababu kubwa zaidi ya kuwa na malengo ni kuongeza faida na mauzo

Hivyo kulingana na sababu hizo za jumla hupelekea kuwa na faida zifuatazo kwenye biashara kupitia malengo

  • Hutoa dira na muongozo wa biashara, yani husaidia mfanya biashara kupita njia sahihi kulingana na mipango yake ya awali bila kuathiri mchakato mzima wa biashara yake
  • Huongeza ufanisi wa biashara, hii pia ni faida kubwa kwani kupitia malengo husaidia kuongeza jitihada na kufanya kazi kwa weledi zaidi hivyo kupelekea ufanisi mzuri
  • Huipa biashara uhai , kwa sababu kupitia malengo husaidia kuwa makini na kuboresha mambo mara kwa mara ili biashara kuendelea kuwa bora
  • Huongeza hamasa, kwamba hufanya mfanya biashara na waajiriwa wake kupata motisha kwa kufanya kazi kwa juhudi kila wanapoona mambo yanaenda kama yalivyopangwa
  • Husaidia kupima mafanikio ya biashara, kwakuwa mara kwa mara mfanya biashara husimama katika malengo yake hivyo huweza kuona kama anapiga hatua au anarudi nyuma
  • Husaida kuongeza mauzo na faida, kwa sababu ya ufatiliaji wa mara kwa mara hufanya uwepo wa marekebisho ya haraka kwa kila changamoto inayotokea ili kutimiza lengo
  • Hupunguza hatari za biashara, umakini wa mfanya biashara mara kwa mara kupitia malengo aliyo nayo hivyo humsaida kuweka sawa makosa ya mara kwa mara haraka
  • Huonesha mchakato mzima wa biashara, husaidia kuwa na mipango ya wazi yenye uhalisia ili kufikia malengo husika
  • Huongeza uzingativu wa biashara kwenye kila hatua inayopitia biashara husika na mfanya biashara kwa ujumla.
malengo ya biashara
Photo by fauxels on Pexels.com

Hatua Za Kupanga Malengo Ya Biashara

  1. Jua malengo unayotaka kutimiza

    Hapa weka aina zote za malengo ila yatofautishe kila lengo na mipango yake ili kurahisisha mchakato na urahisishaji wa kufikiwa

  2. Gawanya malengo ya muda mrefu

    Lazima ujue kwanza lengo la muda mrefu ni lipi ili isaidie mchakato wa malengo ya muda mfupi

  3. Vunja vunja malengo ya muda mrefu yawe ya muda mrefu

    Hapa sasa utagawanya yale malengo yako yote ya muda mrefu katia vipengle vifupi vifupi kwanza yani usibebe lengo kama lilivyo

  4. Andaa mikakati na mipango

    Baada ya kuwa na malengo ya muda mrefu na mfupi sasa panga mikakati sahihi ya kufikia malengo yako yenye uhalisia zaidi

  5. Anza utekelezaji kwa vitendo

    Kupitia mipango na mikakati uliyo jiwekea sasa ingia katika vitendo halisi na utekelezaji wa hatua kwa hatua

Sifa Za Malengo Mazuri Ya Biashara

Ili malengo yaweze kufikiwa ni lazima pia yawe na sifa zake maalumu ambazo huenda sambamba na lengo

Kuna sifa tano za malengo mazuri ambazo zimeainishwa kama ifuatavyo:

  1. Yenye muda maalumu, kwamba lazima kila lengo la biashara lioneshe muda wa mwisho wa kufikiwa ili kuongeza hamasa na ufanisi wa kufanikisha
  2. Yenye uhalisia ,maana yake ni kuwa lazima pia yawe na uhalisia kulingana na ukweli halisi wa mambo na kusiwe na mambo ya kusadikika
  3. Yenye kupimika, hii pia ni sifa ambayo malengo haya yanapaswa kuwa nayo kwa maana kuwa yaweze kupimika mafaniko yake ndani ya muda fulani
  4. yanayo fikika, kwa maana kuwa malengo pia lazima yazingatie ufikikaji wake
  5. Yawe maalumu ,yaani lengo liwe maalumu au moja kubwa bila kuchanganya changanya aina za malengo wakati mmoja na kwenye mipango ya aina moja hii husaidia kuweka mkazo kwa jambo moja kwanza.

Hitimisho

Kwa wafanya biashara wote wadogo au wakubwa suala la kuwa na malengo kwenye biashara ni jambo lisilo kwepeka

Biashara nyingi hufa au kubakia vile vile miaka nenda rudi kwa sababu za kukosa malengo madhubuti

Hii hupelekea biashara nyingi kufanyika kwa mazoea badala ya kukua na kuongezeka thamani yake

Watu wengi hufanya biashara kwa kuangalia faida za muda mfupi ambapo ni chanzo kikubwa cha biashara kutosonga mbele.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Biashara Ya Mahindi Ya Kuchemsha5 Min Read

Next Post

Mbinu Rahisi Za Kufanikiwa Bila Kuchoka Sana7 Min Read

Comments 20
  1. Ninaendelea kusoma ila nna swl,
    Mfn. Kutaka kukuza mtaji wangu maybe uwe double ya uluvyo sasa…hili naliweka kwenye malengo ya muda mfupi au muda mrefu?

  2. Kuna kale kafeeling unakua nako uwe umejiwekea tu malengo twako na utufanikishe 😊😊

  3. Andiko zuri, ila mimi ni mgeni hapa. Je unafanya physical consultations kwa sisi wa Dar madam, au unapatikana wapi?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.