You Can Win If You Want

Wazo La Biashara Ya Mahindi Ya Kuchoma4 Min Read

Utangulizi

Biashara ya mahindi ya kuchoma sio biashara ngeni kabisa nchini Tanzania lakini pia ni miongoni mwa biashara ndogo yenye faida kubwa sana

Watu wengi wanaofanya biashara hii wana uwezo wa kuendesha maisha yao ya kila siku bila kusahau kufanya mambo yenye maendeleo

Wengi hudharau sana biashara ya mahindi ya kuchoma na kuhisi kuwa haina faida sana wala uwezo wa kufanikisha malengo

Wamesahau kabisa kuwa mahindi ya kuchoma ni moja kati ya kiburudisho kipendwacho na watu wengi sana mjini hata vijijini

Japokuwa huuzwa kwa bei ndogo sana lakini mzunguko wa wahitaji na wateja huwa mkubwa zaidi hivyo kufanya faida kupatikana kwa haraka

Mtaji wake wa kuanzia ni mdogo sana na upo ndani ya uwezo wa mtu yoyote mwenye nia ya dhati

Hii hutokana na ukweli kuwa baadhi ya vifaa kama jiko unaweza kuanza na lile la matumizi ya nyumbani la kila siku

Bila kusahau huhitaji vifaa vingi kuanza kuchoma mahindi zaidi ya jiko , wavu na mahindi yenyewe!

Vile vile uhakika wa kuuza ni mkubwa hata kama utaamua kuuzia mtaani kwako au hata nje ya nyumba unayoishi

Pia kutokana na kupendwa na watu bila kusahau bei rafiki kwa wateja imefanya biashara hii kupata mvuto zaidi

Vile vile biashara hii haihitaji ujuzi wala utaalamu wowote wa ziada zaidi ya kuchoma mahindi pekee.

biashara ya mahindi ya kuchoma
Photo by Engin Akyurt on Pexels.com

Sehemu nyingi huuza kipande kidogo cha muhindi wa kuchoma shilingi mia moja na muhindi mzima kuanzia mia 5

Bei huweza kupanda au kushuka kutegemea mazingira,msimu na hata sababu zingine za muuzaji kama ushindani.

Vifaa Vinavyo Hitajika Kwenye Biashara Ya Kuchoma Mahindi

Kwa kawaida biashara ya kuchoma mahindi inahitaji vifaa vichache sana vya kuanzia biashara kama ifuatavyo:

  • Jiko la kuchomea
  • Wavu wa chuma
  • Chumvi
  • Ndimu
  • Pilipili ya unga
  • Mkaa
  • Mahindi
  • Vifungashio kama magazeti

Ukweli ni kuwa biashara hii haina mambo mengi kutokana na uhalisia wake hasa kwa wateja wanao nunua

Sio aina ya baishara inayotaka mteja kukaa hapo hapo kula mahindi aliyonunua na zaidi wateja hupendelea kusimama

Ni chakula rahisi kuliwa katika mazingira yoyote yale hivyo usiwaze kuweka vitu vingi kwa lengo la kuvuta wateja

Ila kama unaweza kupata benchi husaidia zaidi wateja kuvutiwa kukaa hasa wakati wanangoja huduma

Hivyo unaweza kuanza biashara hii hata kwa mtaji wa Elfu 3 tu za kununulia mahindi hasa kipindi cha msimu huwa mengi sana

Kama tayari una jiko na wavu wa kuchomea mahindi , ukishapata uhakika wa wateja utakuza mtaji taratibu kupitia faida unayopata.

Na kama una mtaji mzuri zaidi unaweza kufanya biashara kwa namna ya utofauti zaidi kwa uzingatiaji wa mazingira mazuri.

Sehemu Zenye Wateja Wengi Wa Biashara Ya Mahindi Ya Kuchoma

Biashara hii ina wateja wengi sehemu yoyote ile bila kuogopa kabisa unaweza kuanzisha hata mtaani kwako

Lakini ili kuongeza mzunguko mkubwa zaidi wa biashara yako zingatia maeneo kama:

  • Stendi za dala dala
  • Stendi za mabasi ya mikoani
  • Vijiwe vya boda boda na bajaji
  • Vijiwe vya mazungumzo ya vijana
  • Mashuleni
  • Nje ya vyuo mbali mbali
  • kwenye Masoko
  • Fukwe za bahari
  • Na shemu nyingine zote zenye mkusanyiko wa watu wengi.

Biashara hii zaidi hupendwa msimu wa baridi na mvua hakika wateja wengi hufurahia kutafuna mahindi ya moto wakati baridi.

corn on a grill on a seashore
Photo by Melike Sayar Melikesayar on Pexels.com

Mambo Ya Kuzingatia Kwenye Biashara Ya Mahindi Ya Kuchoma

  • Ununuzi wa mahindi laini yenye ladha
  • Hali ya joto (Moto) yaani mahindi yawe ya moto na epuka kuandaa mahindi mengi na kuyachoma kabla ya uwepo wa wateja
  • Kutokuunguza mahindi kabisa yaani epuka kuuza mahindi meusi
  • Kutokuwa na hali ya uchafu wa aina yoyote kuanzia mazingira na mwili hasa zingatia usiwe unavuja jasho kabisa
  • Kauli nzuri hasa jitahidi kuwa muongeaji sana hufanya mteja atafune muhindi haraka na kuongeza mwingine
  • Muda wa kuanza biashara hasa jioni na usiku, pia unaweza kuanza mchana inategemea na wateja wako
  • Pilipili ya unga isiyo washa sana na ndimu kwa wateja wanopenda.

Hitimisho

Biashara hii ya mahindi ya kuchoma ni biashara isiyotumia nguvu kubwa sana japo ina changamoto chache kama:

Baadhi ya wateja hutaka kujichagulia mahindi wao wenyewe wanayotaka na hii hupelekea kukwazika kwa muuzaji kiasi

Hivyo jitahidi kuwa na subra sana pia nunua mahindi yenye mvuto kwa wateja hasa yale makubwa makubwa.

NB: gharama za mtaji, faida na hata baadhi ya vitu havijawekwa kutokana na sababu kadhaa na ikiwa umependezwa na biashara hii wasiliana nasi kwa kubonyeza link hii.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Uoga Hauzuii Kifo, Unazuia Kuishi1 Min Read

Next Post

Jifunze Kusamehe Hata Kama Hujaombwa Msamaha1 Min Read

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.