You Can Win If You Want

Wazo La Biashara Ya Nguo Za Mitumba8 Min Read

Biashara ya nguo za mitumba

Utangulizi

Biashara ya nguo za mitumba sio kitu kigeni kabisa nchini Tanzania ukizingatia asilimia kubwa ya watu ndio mavazi yao

Yaani nguo za mitumba ni nguo zinazovaliwa sana na watanzania wengi kutokana na urahisi wake wa bei

Pia ni nguo ambazo zinapatikana kwa wingi sana nchini Tanzania mahala popote mjini au vijini na pia,

Kwa mujibu wa tafiti miaka ya hivi karibuni imebainisha kuwa Tanzania ni nchi ya tatu kwenye listi ya kuagiza zaidi nguo za mitumba Afrika

Hivyo hii pekee ni moja kati ya sababu na kigezo kikubwa sana kwa anaepata hofu ya uhakika wa soko

Soko la nguo za mitumba ni soko la uhakika mahala popote nchini Tanzania iwe mjini au hata vijijini ndani ndani

Hakuna mtu ambae havai nguo hata kama kuna hali ngumu ya maisha na kipato kidogo mahala popote

Hivyo suala la uhakika wa wateja sio kitu cha kuhofia kabisa ikiwa kuna nia ya dhati ya kufanya biashara hii.

Lakini pia kuna mitumba ya aina zote, bei aina zote na hata ubora wa aina zote umri wowote na jinsia yoyote

Maana yake ni kuwa biashara hii inaweza kufanywa na mtu yoyote kwa aina yoyote ya kiwango cha mtaji

Kuna mitumba inauzwa mpaka shilingi mia moja za kitanzania masokoni,na ipo ya mpaka shilingi elfu 10 na kuendelea

Hivyo basi kiwango cha ubora wa nguo za mitumba pia hutegemea kiwango cha bei ya ununuzi na mazingira.

biashara ya nguo za mitumba
Photo by Muhammad-Taha Ibrahim on Pexels.com

    Mtaji Wa Biashara Ya Nguo Za Mitumba

    Kama ilivyo ukweli kuwa biashara hii inaweza kuanzishwa kwa kiwango chochote cha mtaji kwa kuzingatia aina ya wateja

    Kitu kingine cha kuangalia linapokuja suala la mtaji ni mazingira husika na kipato cha wanunuaji

    Bila kusahau namna ambavyo mfanya biashara anataka kuendesha biashara yake mfano kutembeza au kukodi fremu

    Wapo wengine huuza nguo za mitumba kwa njia ya mitandao tu kwa kutumia simu zao kama njia ya kupata wateja

    Kwahio mtaji rasmi pia ni muanzaji binafsi amekusudia kuuza kwa mtindo gani haswa na amekusudia kuuzia watu wa aina gani.

    Angalau kuanzia shilingi Elfu 30000 zinatosha kuanza biashara hii kwa anaeanza kujitafuta kuanzia chini

    Kwa maana kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kupata nguo za mitumba kwa mtaji wa 30000 tu na kuanza kutembeza mitaani.

    Kuna ambao hutaka kuanza kwa kununua masokoni (ku point) na wengine hutaka kuanza kuagiza BALO zima

    Wote hawa hawawezi kufanana linapokuja suala la mtaji wa kuanza nao kwa mazingira waliyopo.

    Nguo Za Mitumba Hupatikana Wapi? ( Machimbo Ya Nguo Za Mitumba)

    Kuna sehemu nyingi sana zinapopatikana nguo za mitumba kutokana na ukweli kuwa ni biashara iliyosambaa sana

    Kuna masoko mengi sana ambayo huuza nguo kwa bei rahisi mno kwa bei ya jumla na reja reja mahala popote

    Mfano Jijini Dar es salam kuna soko maarufu kama ILALA BOMA na KARUME ambapo kuna uhakika mkubwa wa nguo

    Lakini pia mikoa na wilaya zote nchini Tanzania kuna wauzaji wa nguo za mitumba wa aina zote .

    Muda Mzuri Wa Kupata Nguo

    Mara nyingi machimbo ya nguo huanza asubuhi sana na wengi huamka mapema kuwahi kuchagua nguo

    Asubuhi huwa kuna uhakika wa kupata nguo nzuri kwa bei ndogo zaidi kwa sababu wauzaji wa mabalo hufungua asubuhi sana

    Hivyo kwa muuzaji yoyote wa nguo hizi anapaswa kuamka mapema sana kuwahi uchaguzi wa nguo

    Angalau kuanzia mida ya sa kumi na moja za asubuhi au mapema zaidi ili kupata nguo nzuri na kwa bei nzuri

    Vile vile kwa wale wanaotaka kuanza na uchaguzi wa balo zima ,yapo mabalo kwa wauzaji wa mitumba ya jumla

    Na pia kuna uwezekano wa kuagiza kutoka China , Uturuki au nchi nyingine yoyote uzuri ni kuwa ni rahisi sana

    Hasa kwa kuzingatia mtandao kama Alibaba na mingine mingi au kupitia mawakala wa uagizaji wa nguo nje ya nchi

    Pia kuna ambao husafiri wao wenyewe mpaka nchi za jirani kununua mabalo ya nguo kwa unafuu wa gharama

    Bei za mabalo huanzia kati shilingi laki 2 na kuendelea kutegemea aina ya nguo na ubora wake

    Kuna nguo kuanzia Grade A, B ,C hizi grade hutegemea ubora wa nguo ,kuna zile nzuri zaidi na MARONYA.

    Aina Ya Nguo Za Mitumba

    Kuna aina mbali mbali na aina zote za nguo za mitumba kwa jinsia zote na umri wowote ule mfano:

    • Mitumba ya watoto
    • Mitumba ya wadada
    • Mitumba ya wakaka
    • Mitumba ya watu wazima
    • Majaketi
    • Mashati
    • Suruali
    • Sketi
    • Magauni
    • Tisheti
    • Nguo za ndani
    • Mashuka
    • Kaptula NK

    Vile vile nguo za mitumba zipo zile za kudumu muda mrefu sana na nzuri mno na zile zisizo na ubora wowote

    Kitu cha kuzingatia ni aina ya wateja na mazingira ya muuzaji.

    Faida Ya Nguo Za Mitumba

    Kama ilivyo kwenye mtaji wa nguo za mitumba kuwa hautabiriki vile vile hata faida haiwezi tabirika

    Kuna muda inawezekana kupata faida kubwa sana kutegemea na mteja au ubora wa nguo na wakati mwingine faida ikawa ndogo

    Kwa wale wanaonunua mabalo mazima changamoto huja kwenye nguo kuchanganywa yani nzuri na mbaya

    Kuna muda nguo nzuri huwa chache zaidi ya zile MARONYA hii huweza kupelekea hasara kubwa zaidi

    Angalau wale wanao point wenyewe huwa na uhakika wa kupata nguo wanazotaka kulingana na aina ya wateja wao.

    Suala la faida kuna muda hupatikana kubwa zaidi kuliko bei ya ununuzi kulingana na mazingira au ushawishi wa muuzaji.

    nguo za mitumba
    Photo by cottonbro studio on Pexels.com

    Biashara Ya Nguo Za Mitumba Kwa Asiye Na Mtaji Kabisa

    Ukweli ni kuwa kuna baishara zinaweza kufanyika kwa wasio na mtaji kabisa na zikawezekana mfano ni hii

    Mtaji sio kikwazo kabisa kwenye biashara na mtu mwenye nia ya dhati ndani ya moyo ya kujikwamua

    Kama imeshindika kupata angalau Elfu 30000 au chini ya hapo kuanza kama mtaji wa biashara kwa anae jitafuta

    Inawezekana kuanza kwa kuuza nguo za mtu mwingine mitaani au mitandaoni kisha kuchukua faida ya juu

    Mfano kuna wauzaji wengi sana wa nguo mitaani wanaotembeza ,ambao hawawezi kukataa kutoa nguo zao kuuziwa

    Hivyo anaehitaji kuanza na hana pesa anaweza kuongea na wale wanaotembeza mitaani nguo zao

    Kisha kuingia makubaliano ya kusaidia kutafuta wateja au kushirikiana kuuza kwa lengo la kuzoea biashara

    Baada ya kuzoea na kujua machimbo, kupata wateja na hata koneksheni mbali mbali ni rahisi kujitegemea.

    Lakini pia inawezekana kutafuta wateja hata bila kutembea na mwenye mtaji mitaani, kwa maana kuwa

    Inatosha kupiga picha nguo na kutafuta wateja kwa njia ya mitandao kama Whattsup business, facebook na instagram

    Mtaji wa kuanza biashara sio kikwazo kikubwa cha mtu mwenye nia ya dhati ya kujishughulisha na kujikwamua.

    Wateja Wakubwa Wa Nguo (masoko)

    Kama tulivyoona kuwa nguo hizi ni pendwa kwa watu wote na rika zote hivyo basi tutaangalia zaidi wateja wakuu

    Tukiondoa jamii nzima kuna wateja ambao ni uhakika zaidi katika ununuzi wa nguo hizi za mitumba

    Hivyo kwa ambae hajui aanzie wapi anaweza kupata mwanga wa aina ya nguo za kuanza nazo kwa urahisi wa soko

    • Wadada na wanafunzi wa vyuo mbali mbali kutokana na ukweli kuwa wadada wengi hupenda kuvaa sana na kubadili mitindo ya nguo wakati huohuo kubana bajeti zaidi hivyo hupendelea zaidi nguo za mitumba
    • Watoto chini ya miaka 7 ,wengi huvalishwa zaidi nguo za mitumba kama namna ya kubana matumizi ya bajeti kwa wazazi wengi

    Kwahio nguo za wadada na watoto zina soko kubwa zaidi kwa anaetaka kuanza biashara hii japokuwa hata nyingine zinauzika pia.

    Mtindo Wa Uuzaji Wa Nguo Za Mitumba

    Kila mmoja huchagua aina ya mtindo anaotaka kutegemea na mtaji alionao kama vile

    • Kuuza kwa jumla mabalo
    • Kuuza kwa reja reja

    Pia eneo na wateja inaweza kuwa kwa:

    • Kutembeza mitaani
    • Kutafuta fremu
    • Kutundika mahala
    • Mitandaoni
    • Masokoni Nk
    grayscale photo of woman wearing hijab
    Photo by Patrick Cristobal on Pexels.com

    Mbinu Za Kufanikiwa Kwenye Biashara Ya Nguo Za Mitumba

    Kuna mambo muhimu ambayo yanaweza kusaidia kwenye kufanikiwa zaidi kwa biashara hii kama

    1. Uchaguzi wa wateja maalumu

      Kuchagua aina ya wateja ambao wanaendana na mtaji au uhitaji wa faida na ubora wa nguo za kuwauzia na hata jinsia au umri maalumu

    2. Kuuza nguo za aina moja au mbili

      Ni vizuri zaidi kuwa na aina moja ya nguo mfano majaketi pekee au nguo za ndani tu na hata magauni tu

    3. Kufua nguo na kuzipiga pasi

      Japokuwa sio lazima sana ila huongeza ubunifu zaidi na hata ushawishi kwa wanunuzi na kupata faida nzuri zaidi

    4. Kuchagua nguo zenye ubora

      Hasa kwa kuzingatia aina ya wateja mfano nguo za mjini huwa tofauti na zile za wanunuzi wa vijijini

    5. Uvumilivu na subra

      Kwa lengo la kujenga msingi mzuri na wateja wa uhakika zaidi

    Hitimisho Na Changamoto Za Biashara Ya Mitumba

    Kama zilivyo biashara nyingine zozote ,changamoto ni jambo lisilo kosekana kwenye biashara aina yoyote

    Hata kwenye biashara hii pia kuna changamoto zake licha ya kuwa na faida nyingi sana za kipato

    Mfano changamoto kama nguo kukosa wateja kwa muda mrefu hasa kwa wale ambao hawakufanya uchunguzi wa wateja

    Kununua maronya mengi zaidi ya nguo za maana hasa kwa wale wanunuzi wa jumla wa mabalo makubwa

    Ushuru mkubwa bandarini hasa kwa wale wanao agiza mitumba nje ya nchi kama China na nchi zingine za mbali

    Na changamoto nyingine nyingi za kawaida kwenye biashara yoyote ile ,jambo la msingi ni kutafuta utatuzi makini

    Bila kusahau uvumilivu na subra ni nguzo ya mafanikio kwenye biashara hii ili kupata wateja wa kudumu na uhakika.

    Share this article
    Shareable URL
    Prev Post

    Mbinu Za Kuishi Na Watu Vizuri6 Min Read

    Next Post

    Mbinu Za Kuondoa Uoga Na Hofu11 Min Read

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    Read next

    Huruhusiwi ku copy. Asante.