You Can Win If You Want

Ajionavyo Mtu Nafsini Kwake Ndivyo Alivyo

Ajionavyo mtu nafsini kwake Ndivyo alivyo

Ajionavyo mtu nafsini kwake Ndivyo alivyo Maana yake ni kuwa namna yoyote unavyojiona kwa ndani wewe mwenyewe ndivyo ambavyo unapaswa kuwa kwa nje

Hata kama nje yako bado hujafikia hata theluthi ya unavyojiona ndani yako, nafsi yako na ulimwengu wa roho ndio,

Hukupa picha halisi ya vile unapaswa kuwa kwa nje bila kujali vikwazo vingine vyovyote

Haijalishi maisha yako ya sasa wala maisha yako ya nyuma ila kinachoangaliwa ni namna wewe ulivyo ndani yako

Kama unajiona kwa ndani ni kiongozi wa siasa mkubwa hata kama kwa sasa upo kijijini unalima na hakuna anaekujua

Amini kuwa umezaliwa kuwa kiongozi unae muona ndani yako na inawezekana kufikia hilo

Inawezekana kwa sasa unaishi maisha ya kuunga unga na huna muelekeo wowote lakini kwa ndani yako unajiona ni tajiri mkubwa sana basi amini kuwa umezaliwa kuwa hivo

Pengine kwa sasa unafanya mambo maovu sana yaliyo kinyume na maamrisho ya Mungu

Lakini kwa ndani yako unajiona ni kiongozi mkubwa sana wa Dini jua kuwa wito na kusudi lako la kuumbwa lipo hapo hapo.

Unapaswa Kuwa Ujionavyo Nafsini

Bila kujali maisha na mapito yako ya sasa kitu pekee ni kupigania kutimiza kile unachokiona ndani yako

Kama unajiona wewe ni Daktari mkubwa hata kama kwa sasa unauza mahindi amini inawezekana

Pengine kwa ndani unajiona ni muandishi mkubwa wa vitabu hata kama kwa sasa unauza mgahawa amini kuwa unaweza

Endapo kwa ndani unajiona ni Raisi ajae hata kama kwa sasa hujulikani kabisa katika nafasi yoyote ya uongozi jua kuwa umezaliwa kuwa Raisi

Haijalishi ugumu wake wala changamoto zake kikubwa ni kuwa unapaswa kuwa vile unavyojiona kwa ndani ili kutimiza kusudi la kuumbwa kwako

Hakuna jambo rahisi wala hakuna jambo gumu hapa Duniani ila kila jambo linaongozwa na Imani ya mtu

Imani yako ikiwa ndogo jambo lazima litakuwa gumu hata kama linawepesi ndani yake

Na endapo Imani yako ikiwa kubwa basi kitu chochote huwa chepesi hata kama kina ugumu ndani yake.

Umezaliwa Kwa Kusudi Maalumu

Kila mmoja ameletwa Duniani kwa lengo la kufanya kitu fulani ndani ya kusudi fulani kama ajionavyo mtu nafsini

Hakuna aliyeletwa kwa bahati mbaya wala kusindikiza wengine kwenye maisha yake

Wote tupo kufanya kitu maalumu na taswira nzima ipo ndani yetu sisi wenyewe

Yani ndani yako tayari una kila kitu ,maagizo na maelekezo yote ya kufanya na kuishi ndani ya kusudi la kuumbwa kwako

Usiogope ukubwa wa taswira unayoiona kwa ndani kwasababu ipo kwa ajili ya kukutumikia wewe

Iagize taswira yako ikupe kile unataka kutimiza na utaona namna maisha yanajiendesha ndani ya maana nzima ya maisha yako.

Pambana Kufikia Unavyojiona Nafsini

Hakuna mtu atakae kuja kukusaidia kwasababu kila mmoja ana twasira yake tayari

Wewe mwenyewe ndio unapaswa kujiinua na kukimbizana na hio taswira ya ndani mpaka itoke kwa nje

Usikubali ubaki kama bunzi kwenye muhindi, maana kama hutaishi ndani ya ulivyo basi ni kama umepoteza maana nzima ya maisha yako

Maisha ni mazuri sana na hayapaswi kuwa na maumivu yoyote ila maumivu huja kwasababu ya kulazimisha kuishi nje ya kusudi lako

Mungu ameshatupa kila kitu na hakuna kitu cha kumuomba tena bali unapaswa kutumia kile ulichopewa na kukimiliki vile unataka ili kikupe vyote vilivyobaki.

Huwezi Kuwa Zaidi Ya Ujionavyo Nafsini

Kamwe hutoweza kuwa zaidi ya ujionavyo nafsni kwako, kama unajiona hufai na upo kwa ajili ya kutegemea wengine basi jiandae kuwa hivyo

Hata ukipewa kila kitu cha kukusaidia kama unaona huwezi jua kuwa hutoweza kabisa

Kama unaamini unaweza kuwa aina ya yule aliye ndani ya nafsi yako lazima utakuwa hata kama mzingira yote hayakusapoti kabisa.

Hatua Za Kuishi Kama Ujionavyo Nafsini

  1. Gundua taswira yako

    Kwa kujiuliza ndani yako unajionaje na unataka kuwa nani

  2. Weka nia

    Nia na dhamira ya kuwa lazima ufikie vile unavyojiona kwa ndani bila kujali changamoto za nje

  3. Andaa mipango

    Kupitia taswira yako ya ndani kwa namna yako mwenyewe panga mikakati utaanzaje na utafanyaje kufikia unavyojiona kwa ndani yako

  4. Anza utekelezaji

    Kupitia mipango yako kidogo kidogo kila siku bila kuacha kwa kujisogeza karibu na kila unachokiona kitakufaa na kukusaidia

  5. Usirudi nyuma

    Utakutana na vikwazo vingi vya nje vya kila aina jambo la msingi ni kuendelea na kusimama katika unachokifanya na kukiamini tu.

Mambo Ya Kuzingatia Ili Kufikia Ujionavyo Nafsini

  • Ondoa uoga
  • Jiamini
  • Epuka kuomba ushauri sana hasa kwa watu ambao hawafanyi kile unachokitaka
  • Weka mikakati hata kama unaona itakuwa migumu kuitimiza
  • Jenga imani kubwa
  • Simamia msimamo wako
  • Fanya kila siku angalau kitu kidogo
  • Jifunze mambo mengi kuhusu vile unata kuwa na tafuta taarifa sahihi kila mara
  • Jisogeze kwa watu chanya wanaofanya mambo yale unayoyataka
  • Jikane maisha yako ya nyuma na usikubali mambo ya nyuma yakuendeshe
  • Jitoe kwa kila kitu na usikate tamaa kabisa wala usirudi nyuma.

Hitimisho

Amini kuwa Ujionavyo Nafsi Ndivyo Unapaswa kuwa na kuishi maisha hayo unatakiwa kuzingatia maagizo ya ndani yako ili uishi ndani ya maana na kusudi la kuumbwa kwako

Usiige maisha ya watu wengine wala usikubali kupangiwa mambo ya kufanya kwenye maisha yako na watu wengine

Kwasababu kila mmoja ameletwa kwa kusudi tofauti na mwingie kama vile ajionavyo yeye mwenyewe

Ondoa uoga na jiamini kisha pambania kile kilichopo ndani yako tu.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Mbinu za kutimiza Malengo

Next Post

Orodha Ya Biashara Ndogo

Acha Comment Yako

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.