You Can Win If You Want

Fahamu kuhusu tahajudi (meditation)

Utangulizi

Tahajudi au meditation ni kitendo cha mtu kufikia kiwango cha juu cha utulivu wa akili kutokana na sababu yake maalumu

Kitendo hiki huambatana na akili kwasababu akili ndio ina simamia na kuendesha maisha ya mtu yoyote

Ukiweza kuitumia akili yako vizuri basi utapata chochote unachotaka na utaishi kwa kusimamia mazingira yako yote ya ndani na nje ya mwili wako

Hii inaweza kufanywa na mtu yoyote wakati wowote kwa sababu mbalimbali lakini lengo kubwa zaidi ni kupata utulivu na amani ya ndani kabisa kupitia akili na ubongo

Jambo hili lipo sehemu nyingi na asilimia kubwa ya watu wa mataifa mbalimbali hufanya kwa kuambatanisha na mambo ya KIIMANI

Kama Dini na Miungu mfano rahisi ni dini ya buddhism ,Jaininism,Hinduism na hata dini ya kiislamu.

jifunze tahajudi

Image by Ralf Kunze from pixabay.

Faida za kufanya tahajudi

Kuna faida nyingi sana za kufanya tahajudi au meditation kwa kila mtu tukiondoa faida na sababu za kidini

Leo tutangalia faida chache zinazoambata na sababu za kiafya.

  • Huongeza kiwango cha amani Ijue nguvu iliyo ndani yako
  • Huondoa mawazo mabaya
  • Husaidia kupata furaha ya ndani
  • Huongeza uwezo mkubwa wa kufikiri na kutatua changamoto
  • Huboresha afya ya akili
  • Huongeza ufanisi wa kazi na maisha na kupelekea mafanikio makubwa
  • Huboresha mfumo wa mzunguko wa damu na kupunguza matatizo ya afya kama presha ,moyo,na hata mfumo wa chakula tumboni
Huongeza kiwango cha amani

Kutokana na changamoto za maisha ya kila siku kuna wakati hujikuta amani ya ndani inaondoka na kujihisi hali ya kupoteza muelekeo na hata wasiwasi mkubwa ndani ya nafsi

Ukifanya tahajudi husaidia sana kuweka akili yako sawa na kurejesha hali ya utulivu wa ndani kwa kukuondolea wasiwasi hata kukurudisha katika utambuzi wako binafsi.

Huondoa mawazo mabaya

haya ni mawazo kama kujikataa, kukata tamaa,kujidhuru ,kuhisi kuelemewa na hata hali ya kujiona kama umefika mwisho wa majaribu yako

Na kama huwezi tena kufanikisha jambo lolote mbele yako, ukifanya tahajudi kupitia matatizo yako kwa lengo la kujipata upya

Husaidia kuifungua akili yako upya na kukuondolea uzio wote uliojengeka mbele yako kwenye akili

Utaanza kuona mwanga mpya na njia mbali mbali zitafunguka katika akili yako za kukabiliana na matatizo uliyonayo.

Husaidia kupata furaha ya ndani

kuna nyakati za maisha kutokana na sababu mbalimbali furaha huondoka na kuona kama maisha hayana maana tena

kumbuka furaha yako ipo ndani yako mwenyewe na haihusiani kabisa na mazingira ya nje ,mtu au vitu

Hivyo kupata au kukosa furaha husababishwa na namna unavyofikiri kwa ndani au namna unavyopokea tatizo linalokukabili

Ili kuweza kuwa na furaha lazima uwe na mawazo chanya kila mara na ubadili mtazamo na namna unavyochukulia mambo

Kwahio ukifanya tahajudi husaidia sana kukupa utulivu ndani ya akili yako na ubunifu wa suluhu mbalimbali za changamoto

Ikiwa pamoja na kukupa furaha nyakati zote bila kujali manzigira yako ya nje.

Huongeza uwezo mkubwa wa kufikiri na kutatua changamoto

Kama ilivyo ukweli kuwa akili zetu zimeumbwa zikiwa na majibu ya changamoto zote

kuweza kutatua changamoto huambatana na kiwango cha kufikiri cha mtu binafsi

Kila binaadamu ana asilimia mia moja za akili, ila matumizi ya akili yametofautiana kutokana na uwezo wa kufikiri wa kila mmoja

Sasa tahajudi husaidia sana kuboresha mfumo mzima wa akili ya mtu yoyote na kumuongezea matumizi ya akili yake kwa kila jambo analofanya.

Huboresha afya ya akili

Watu wengi kutokana na sababu mbalimbali za maisha ya kila siku wamekumbwa na tatizo la afya ya akili zao

Kuwa na shida ya afya ya akili sio lazima mtu awehuke kabisa ,kuna watu wengi wapo sawa kwa muonekano wa nje

Na wanafanya mambo yao ya kila siku vizuri kabisa na wengine hata ni viongozi wakubwa ila akili zao zina shida

Utangundua ukiongea nae kwa masaa machache sana kuwa hayupo sawa kichwani hata kama ana maisha mazuri sana

Au hata matendo yake anayofanya huwa hayaendani na umri wake wala nafasi yake katika jamii

Sasa tahajudi husadia sana kuweka akili sawa ni kama vile kuibusti akili au kuifanya ijizime na kujiweka sawa upya

Mfano rahisi ni simu au kompyuta kuna muda inatakiwa kufanyiwa restore au re start ili kuweka mifumo yake sawa ya kiufanisi.

Huongeza ufanisi wa kazi na maisha hivo kupelekea mafanikio makubwa

Kama ilivyo ukweli kuwa tahajudi husaidia sana katika kuweka akili sawa na kuongeza uwezo wa kufikiri

Kwa maana hiyo uwezo wa kufikiri ukiwa juu na hata ufanisi utakuwa juu iwe kwenye kazi unayofanya hata biashara na mafanikio yataongezeka.

Huboresha mfumo wa mzunguko wa damu na kupunguza matatizo ya afya kama moyo,presha na hata mfumo wa chakula tumboni

Hapa sasa kupitia tahajudi magonjwa mengi sana yanayohusiana na msukumo wa damu hutatulika kwasababu tahajudi inahusisha matumizi ya ubongo

Akili na ubongo vikitenda kazi sawa sawa basi maradhi mengi hupungua hasa yenye uhusiano wa moja kwa moja na ubongo

Pia tahajudi inapoleta amani huambatana na kuweka mifumo sawa ya ndani ya mwili hivo hali ya msongo wa mawazo na wasiwasi hutulia na kupelekea maradhi kama presha kutulia.

fahamu kuhusu meditation

Maswali yanayoulizwa zaidi

Je tahajudi ni uchawi?

Hapana tahajudi sio uchawi kabisa na haihusiani na imani za ishirikina ila inasaidai kuunganisha mtu kupitia asili yake ya ndani na mazingira yake ya nje

Je naweza kufanya tahajudi hata kama sina imani ya kidini

Ndio unaweza kufanya tahajudi (meditation)hata kama hufungamani na imani yoyote

Je tahajudi (meditation) husaidia kupata utajiri?

Tahajudi inasaidia kuongeza uwezo wa kufikiri na uwezo wa ufanisi hivyo husaidia katika kuongeza ubunifu mkubwa na kuleta mafanikio kwenye kitu unachofanya

Naweza kufanya tahajudi sehemu yoyote?

Ndio unaweza kufanya tahajudi sehemu yoyote kikubwa zingatia utulivu wa eneo

Je tahajudi inasaidia kusahau mambo ya nyuma?
Ndio kama utakusudia kusahau maumivu ya nyuma na kutamani kuanza upya tahajudi husaidia kufanya akili yako kukupa mawazo mapya

Mambo ya kuzingatia ili kufanya tahajudi (meditation)

Ili uweze kufanya tahajudi kwa mtu ambae hujazoea na unaanza kujifunza zingatia mambo haya

  • Eneo tulivu
  • Usiri
  • Utulivu wako binafsi
  • Nia na jua nini unataka

Eneo tulivu

Hakikisha kuwa eneo unalotumia kufanya tahajudi halina kelele kabisa na ukiweza fanya usiku sana au asubuhi sana au muda wowote unaotaka lakini kusiwe na kelele zozote.

Usiri

Wakati unafanya jitahidi uwe mwenyewe na epuka watu kujua au kuona nini unafanya na ikitokea umeonekana kwa bahati mbaya tafuta namna ya kuoesha kuwa hukuwa unafanya tahajudi.

Utulivu wako binafsi

Hapa ondoa kila kitu kitakachokufanya ukose utulivu mfano simu yako unaweza kuzima kabisa na hata mawazo yako ukayakusanya na kuyapuuza kwa muda mpaka pale utakapomaliza.

Nia na jua unachotaka

Lazima uweke nia moyoni kwanza na ujue lengo la tahajudi yako hii itakusaidia kufanya kwa uhakika na kuona matokeo haraka.

Jinsi ya kufanya tahajudi (meditation)

Kufanya tahajudi sahihi kama bado unajifunza inaweza kuwa changamoto kidogo
Lakini ukiwa na nia ya dhati na kujitahidi kufanya mara wa mara utaweza kufanya kwa usahihi

  1. Nia

    weka nia ya dhati ndani ya moyo wako na sema nini hasa lengo la kufanya tahajudi yako

  2. Kaa mkao unaokupa uhuru

    unaweza kulala chali kwa kuangalia juu ukiwa umejinyoosha na kulegeza mwili wako wote

    Au ukakaa mkao ambao utakuwa uhuru wa kukaa muda mrefu bila kuumia wala kujigeuza geuza

  3. Fumba macho yako ya kupumua kwa nguvu mara tatu

    Kisha anza kujitahidi kutowaza kitu chochote kingine zaidi ya kile unachotaka
    Kwa kujiruhusu kuingia ndani ya mawazo yako na kutawala akili yako tu

  4. Jipe muda


    Endelea kutulia na kutafakari kwa kina unachotaka kulingana na nia yako taratibu hata kama utajikuta mawazo yanahama

    Endelea kujipa muda ,tulia na fanya angalau kwa dakika kuanzia ishirini na usizidi dakika thelathini

  5. Rudisha mawazo taratibu

    Baada ya dakika ishirini au thelathini anza kurudi katika hali ya kawaida taratibu na fumbua macho yako

Hitimisho

Tahajudi (meditation)inapaswa kufanyika mara kwa mara hata ikiwezekana kila siku kwa dakika chache ili kuweza kupata matokeo mazuri

Yani huwezi kufanya mara moja na kuona matokeo sahihi, ila lazima ujitoe na iwe sehemu ya ratiba yako ya kila siku au kila mara

Ikiwa hutoona matokeo haraka usiogope kwani huchukua muda kuanza kujihisi vile umekusudia, jambo la msingi ni kutokata tamaa.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Kurudisha thamani ya biashara yako

Next Post

Jifunze kujiajiri

Acha Comment Yako

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.