Jifunze kuwaacha waende watu uwapendao ili uweze kupata amani na furaha ya maisha
Watu wengi imekuwa mtihani mzito kukubali kuwa wanapaswa kuwaruhusu wawapendao kuondoka kwenye maisha yao
wakati mwingine kuwaacha waende ni njia ya kuonesha kuwa unawapenda, unajali na kuheshimu maamuzi yao
Watu wengi hujikuta wakikubali uhalisia wa kuwaacha watu waende baada ya muda mrefu sana kupita bila wao kujua kuwa walipaswa kuwaachilia mapema zaidi
Baki na somo na jifunze kuwaacha waende
Kuna ambao huja kwenye maisha yako kukutumia kutimiza malengo na mahitaji yao
Huondoka wanapoona huna faida nyingine kwao
Mateso na maumivu unayopitia hayakutakiwa kuwa kwa kiwango hiko
Ila kwavile ulilazimisha kubakiza watu ambao ulipaswa kuwaacha waende muda mrefu kwenye maisha yako
Kila anaekuja katika maisha yako, huja kwa nyakati maalumu na lengo maalumu
Muda wake na lengo linapotimia asili humuondoa kwako
Hakuna anaekuja kwa bahati mbaya hata kama umejuana nae siku moja
Na hakuna anaelazimika kubaki milele kwako ili wewe uweze kuishi
Unaweza kubaki mwenyewe
Kitu pekee cha muhimu ambacho binaadamu yoyote hawezi kuishi bila kuwa nacho ni hewa ya “OKSIJENI”
Watu wote unaowaona katika maisha yako kwa nyakati tofauti iwe umekutana nae njiani, kifamilia (uzao), kimazingira au hata sababu nyingine yoyote
Wote hao wapo kwa nyakati sahihi, lengo sahihi na wanapaswa kuondoka katika wakati sahihi
Kulazimisha wabaki wakati muda wao umekwisha ndio chanzo kikubwa cha msongo wa mawazo,
Kujidhuru, kudhuru wengine, kuchanganyikiwa, Vifo, na madhara mengine mengi ambayo yanaepukika kwa kujua muda wa kuachilia
Sababu za watu kuja kwenye maisha yako
- Kukufundisha jambo fulani kama fursa, mafunzo ya kimaisha nk
- Kukuvusha katika nyakati fulani kama nyakati za huzuni nk
- Kukusaidia kitu fulani kama mawazo au malighafi na hata pesa
- Kukuinua katika kiwango fulani kama kielimu, kibiashara nk
- Kukupa furaha ya muda (mrefu au muda mfupi)
Watu wote hao Haijalishi kiasi gani umewazoea, umewapenda, au umuhimu wa kuwa nao ni mkubwa
Kamwe hupaswi kulazimisha wabaki katika maisha yako pale tu muda wao wa kuondoka unapofika

Kuna watu huondoka kwa sababu za kiasili kama “kifo”,
Hupaswi kulia kila siku kwasasabu tu ulifiwa, kumbuka somo walilokuachia shukuru na waache wapumzike salama
Jua hakuna atakae baki na wewe milele hivyo jifunze kuwaacha waende
Na wapo wanaoondoka kwa sababu za kimifumo ya dunia kama,
mahusiano kuvunjika, watoto wako kukutenga, ndugu kukukataa, marafiki kukuchukia, na mambo mengine mengi
Hutakiwi kuumia na kutumia muda wako mwingi kuwafikiria chukua somo walilokuachia na acha waende wakasadie au wakasaidiwe na wengine
Kwenye maisha kila mmoja wetu ana kila kitu cha kumfanya aishi bila utegemezi wa moja kwa moja kutoka kwa mtu mwingine hata kama huyo mtu ni mzazi wako
Tunapaswa kutegemeana ili kuishi lakini sio utegemezi wa ukaribu, mfano tunategemeana katika ufanyaji wa kazi mbalimbali, uzalishaji, huduma za kijamii na kadhalika
Lakini sio utegemezi wa kwamba bila fulani nitakufa na siwezi kuishi
Bila baba au mama siwezi kuishi, bila mwanangu siwezi kuishi, bila mwenza au mpenzi siwezi kuishi, bila rafiki yangu fulani siwezi kuishi au mtu mwingine yoyote
Kwenye maisha unaweza kuishi bila mtu yoyote kuhusika moja kwa moja katika maisha yako
Hivyo jifunze kuwaacha waende muda wao unapofika
Jiandae kwa kupokea watu bora zaidi
Unaweza kuachwa na mwenza wako, ukatumia muda mwingi kumlazimisha asiondoke kumbe unapoteza muda ambao ulipaswa kujiandaa kwa mwenza bora zaidi atakaekuja mbele yako
Pia ulipaswa kutumia makosa ya mwenza anaeondoka kujifunza na kuwa bora kwa yule anaekuja baadae
Unaweza kulazimisha rafiki abaki kwenye maisha yako kumbe alikuja kukufundisha kuwa usiamini watu kupitiliza, na unapaswa kuchukua somo lako na kungoja rafiki mwingine
Unalazimisha kubaki na wazazi wako kumbe ulipaswa kuacha waende na wewe kujua thamani ya kujitegemea katika maisha yako

Kuna wale ambao huja kutunyanyua na kutuandaa kwa fursa za baadae kupitia ushauri, maoni na mawazo yao
Hivo tunapaswa kubaki na funzo na kuwaacha waende muda wao unapokwisha
Ijue thamani yako, wewe ni mtu muhimu sana na hujaletwa duniani kuishi kwenye maisha ya mtu mwingine
Dalili za kujua kama unapaswa kuacha waende
Ukiona baadhi ya dalili hizi katika uhusiano wowote ulionao basi jifunze kuachia nafasi yako kwao
- Mawasiliano kupungua bila sababu za msingi
- Kauli mbaya zisizojali hisia zako
- Waache waende ukiona makosa na maudhi ya mara kwa mara
- Hakuna tena uchangamfu wa awali
- Kuonekana kero kwenye baadhi ya vitu
- Thamani yako inashuka na huoni umuhimu wako kwao tena
- Kutengwa kwenye mambo ambayo awali ulipewa kipaumbele na kutafutwa wakati wa shida
- Kutumia nguvu kubwa kuwa karibu yao
Kuna dalili nyingi sana ila hizo ni baadhi ya dalili utakazoona na kupaswa kuacha waende haraka sana kabla hujaumia zaidi
Mawasiliano kupungua bila sababu za msingi
Hapa unaanza kugundua kuwa hakuna idadi simu wala meseji ulizozoea kuona kwa siku, wiki au mwezi
Unagundua hata unapojaribu kuwatafuta hukupa sababu ambazo hazina mashiko kama vile ubize,
Ipo hivi hakuna mtu ambae yupo bize katika kuwasiliana na mtu muhimu kwake isipokuwa vipaombele
Utaona ukipiga simu haipokelewi haraka na ikipokelewa utapewa dharura kuwa utatafutwa baadae
Meseji hazijibiwi mapema au hata kutojibiwa kabisa
Kauli mbaya zisizojali hisia zako
Watu wanaotamani ubaki katika maisha yao siku zote hutumia kauli za unyenyekevu na kauli ambazo hazitakuumiza kabisa
Ikitokea wamekukwaza huomba msamaha haraka na hujitahidi kutorudia tena
Ikiwa kinyume na hapo, ndugu yangu waache wende tu kwa usalama wa moyo na maisha yako
Lakini pia wapo ambao hutamka wazi kuwa hawakuhitaji ila kwakua unahisi bado unawahitaji,
Utalazimisha hisia zako ziamini kuwa ile Kauli ilikuwa ya bahati mbaya tu
Waache waende ukiona makosa na maudhi ya mara kwa mara
Utaanza kuona unakosewa kila mara na hata ukiwaambia hawajali wala kuonesha kuguswa kama awali,
Jua tu hapo muda sahihi wa kukusanya mabegi umefika na waache aende
Hakuna tena uchangamfu wa awali
Ile hali ya uwepo wako kuwa kama baraka kwao itapungua kwa kiwango kikubwa,
Kiasi cha kuona kabisa kuna shida mahala hapo waache waende
Utaona hata ukiwa nao hakuna furaha wala hali ya kuongea sana kama mwanzo na hata ukiaga unaruhusiwa haraka sana
Kuonekana kero kwenye baadhi ya mambo
Zile nyakati za kwenda kula bata na nyakati za furaha kwao utashangaa huambiwi tena
Wala hualikwi na ikitokea ukauliza utapewa jibu litakalo kufanya ujione wewe ndio mwenye makosa
Thamani yako inashuka na huoni umuhimu wako tena
Utaanza kujiona huna faida tena kwao maana mambo mengi ya awali hushirikishwi
Huulizwi tena maswali wala kuambiwa kuchangia maoni na mawazo yako hasa katika vitu vya msingi vinavyogusa maisha yao
Kutengwa kwenye mambo ambayo awali ulipewa kipaombele na kutafutwa wakati wa shida
Hapo waache tu waende moja kwa moja kwa moja wala usiwe king’ang’anizi kabisa
Maana mambo yapo wazi kuwa sasa huna tena ushawishi wala umuhimu wowote
Kitendo cha kulazimisha mambo Ndio maumivu yanakuwa makubwa zaidi
Lakini pia unapoona nyakati zao za huzuni na matatizo wewe Ndio kimbilio Lao na changamoto zikiisha huwaoni unapaswa kujifunza kuwaacha waende
Kutumia nguvu kubwa kuwa karibu yao
Hapa sasa ndio utajihisi kama hali ya kujipendekeza kwao
Unaweza kutumia nguvu ya pesa au hata muda na maongezi lakini bado muitikio unakuwa mdogo sana na hakuna thamani yako yoyote inayoonekana
Unacho paswa kufanya ni kwaacha waende kwani muda wako kwao umekwisha
Kuendelea kulazimisha wabaki ni kujisababishia maumivu makubwa zaidi kuliko vile ambavyo ungeumia mapema
Utajikuta unapoteza muda wako zaidi, muda ambao ungefanya jambo lingine na kukutana na watu wengine wazuri zaidi
Utatumia pesa na malighafi zako kwa wakati ambao sio sahihi na kwa watu ambao sio sahihi
Na kupelekea maumivu kuzidi kiwango ambacho ungeyapata awali kama tu ungekubali mapema kuachilia waende
Faida za kuacha waende
- Itakuepusha na majuto makubwa
- Itakusaidia kutoumia sana na kukupa amani haraka
- Itakupa nafasi ya kukutana na watu wazuri zaidi mapema
- Itawapa nafasi wanaoondoka kufurahia maisha mengine
- Itawafanya wanaoondoka kukuheshimu zaidi na kuona umuhimu wako ukiwa mbali nao
- Itawapa nafasi ya kuchagua kama unafaa kuwa nao au hufai
- Itakusaidia kupata Msaada wakati mwingine kutoka kwao kwani hmtaachana kwa maumivu na migogoro mikubwa
- Itakupa nafasi ya kuijua na kulinda thamani yako
- Itakusaidia kuziona fursa kubwa zaidi mbele yako
- Utajifunza kutumia muda wako kwa watu wengine vizuri na kujiandaa kwa lolote la baadae
Hitimisho
Usikubali kuishi kwa majuto, usiishi kwenye maisha ya watu wengine wala kulazimisha watu kubaki na wewe. Maisha yanapaswa kuendelea kwa namna yoyote ile iwe wapo au hawapo, hivyo tumia muda wako vyema.Pia soma mbinu za kusahau Mambo ya nyuma na kuanza maisha mapya
Comments 1