You Can Win If You Want

Kiwango cha umasikini na hamasa

Kiwango cha umasikini huanzia kitandani

Kiwango cha umasikini ni kipimo kinachokuonesha hali ya umasikini uliyonayo

Ukitaka kujua kiwango cha umasikini wako anza na kitanda unacholalilia

Ukiwa hapo kitandani fanya tathmini ya kitanda chako, godoro, mto hata mashuka unayotumia!

Kisha geuza macho angalia juu ya paa la nyumba yako au yenu

Endelea kuangalia mazingira ya chumba chako kizima yakoje

Halafu inuka nenda nje ya chumba na kagua mazingira ya vyumba vingine na eneo lote kuzunguka nyumba

Malizia kwa  kuangalia majirani wanaokuzunguka

Nyumba zao, maisha yao na mazingira yao yote.

Fanya maamuzi kuanzia kitandani

Ili uweze kubadili maisha yako jifunze kujipa hamasa kupitia kitanda chako

Kama unaona uvivu kuinuka na  kuchukua hatua yoyote ya kubadili maisha yako basi anza na kitanda chako

Jiulize hivi kitanda changu kinasapoti niendelee kulala? au kinanihamasisha niinuke nikapambane?

Kuna muda watu huweza kulala sana na kupotezea kabisa kufanya jitihada za kujikwamua wakati huo huo vitanda vyao vinawahimiza kuamka

Unakuta watu wanaamua kukaa nyumbani kwao bila kazi ikiwa nyumba yao inawapa ishara za kupambana

Unalazimisha kukaa bila kuhangaika ikiwa majirani zako na mazingira yanayokuzunguka yanakuonesha kabisa fanya jambo!

Kiwango cha umasikini na hamasa

Hakuna nyumba mbaya wala mazingira mabaya

Endapo umeridhika na kitanda chako, chumba na mazingira yako kutoka moyoni basi endelea na kile unachoona ni sahihi

Lakini kama kitanda na kila kinachokuzunguka kinakuhimiza kujituma zaidi basi tumia hio kama Hamasa yako.

Geuza kitanda kuwa hamasa

Kama unaona uvivu wa aina yoyote basi tumia kitanda chako kama hamasa mpya

Maana asilimia zaidi ya 70 kitanda huonesha kiwango cha umasikini ulionao

Hapa sisungumizii kitanda cha ndugu yako! au nyumba ya ndugu yako!

Namaanisha kile ulichonunua wewe kwa pesa halali ya jasho lako

Au kile ulichokulia katika nyumba ya kwanza ya familia yako

Simaanishi kitanda cha gharama ulichonunuliwa na mtu mwingine yoyote

Wala kitanda unachotumia mahala ambapo hapahusiani na nyumbani kwako au kwenu.

Mzingira yako ni hamasa

Aina ya chakula unachokula kwa siku, mavazi unayotumia,mfumo mzima wa maisha na kila kinachokuzunguka

Vinatosha kuwa hamasa katika kupambana kwako

Usikubali kuridhika ikiwa vitu vyote vinakuonea huruma!

Kwanini uridhike kwa mlo mmoja usio na afya kwa siku?

Usije kuridhika kwa kuvaa nguo za mtumba kila siku!

Unawezaje kutuliza akili ikiwa hata  maisha ya hapo unapokaa unaogopa kuleta mgeni kwa kuona aibu?

Mazingira na umasikini

Aina ya marafiki zako ni hamasa kubwa

Marafiki ulionao wanatosha kukufanya uinuke na kufanya jambo

Kuwa na marafiki ambao hawawezi kukusaidia hata shilingi laki 1 ya haraka inapotokea tatizo kubwa hilo ni tatizo lingine!

Yani  wote wameajiriwa au wanafanya kazi za malipo ya posho!

Wale ambao hawana kazi na wanashinda vijiweni!

Marafiki ambao hawana Ushauri wowote zaidi ya kushabikia mpira na starehe

Usikubali kuwa na rafiki ambae hawezi kuwa kukupa mawazo chanya ya maendeleo

Yule ambae kila siku anaishi kama jana, hajui afanye nini au abadili nini

Kataaa ukaribu na mtu ambae hajawahi hata kuwaza mafanikio makubwa wala mbinu za kujikwamua

Tengeneza urafiki na mtu mwenye kufikiria mbali na anaejua nini anataka katika maisha yake hata kama leo hii bado hana chochote.

Ukoo wako ni hamasa zaidi

Ikiwa upo katika ukoo ambao hata matatizo kama misiba na maradhi lazima mchangishane hio inatosha kukupa hamasa

Ukoo ambao kuna historia ya mtu aliye poteza maisha kisa kukosa pesa za matibabu!

Kama unajua ukoo wako hakuna aliye fanikiwa kufika mafanikio ya juu iwe Elimu, biashara hata kitu chochote basi pambana sana

Usibweteke ikiwa ukoo wako wote mkikusanya kila mnachomiliki haifiki thamani hata ya kuwalisha mwaka mzima bila kufanya kazi kabisa

Ndugu yangu familia na ukoo wako tu Vinatosha kukufanya uinuke na kuanza upya

Acha kuishi kimazoea na usikubali kabisa kuwa wa mwisho katika utafutaji

Ni bora utafute ukosefu kuliko kuacha kutafuta kabisa.

Maisha hayataki hamasa za nje wala motisha za watu wengine

Hao “motivation speakers” (wahamasishaji) sio kitu kitakufanya kubadili maisha yako

Ikiwa wewe mwenyewe huoni kitu cha kukupa hamasa kupitia maisha yako binafsi

Usipoteze muda kuhudhuria vikao na semina za kila siku kwa lengo la kutafuta hamasa

Vitabu unavyonunua kila mara sio sababu ya wewe kutajirika au kuanza utekelezaji.

Tumia maisha yako iwe hamasa kuu

Fanya mazingira yako kuwa sababu kuu na zenye uzito wa wewe kutenda na kutochoka kupambana.

Tengeneza chuki na kitanda chako

Kila unapoamka asubuhi au unapotaka kulala usiku jenga chuki na eneo unalo tumia kulala

Jiambie nachukia sana kutumia kitanda hiki, chumba au mazingira yako yote

Sema kwa hisia na uchungu kuwa utafanya kila unachoweza kubadilisha kila kitu kwenye maisha yako.

Jenga chuki na marafiki zako

Hao marafiki ambao umeona kabisa hawakufikishi popote

Wachukie! Sio kwa ubaya bali kwa mawazo chanya tu

Sema kuwa sitaki tena marafiki watakao nifanya nishindwe kimaisha

Na weka nia moyoni kuwa utakuwa miongoni mwa marafiki wanaojitambua na kujua nini wanataka hapa Duniani.

Hujaja Duniani kuwa msindikizaji

Usikubali kusindikiza wengine wewe sio bendera

Umeumbwa kwa kusudi maalumu na unapaswa kufanya kitu kupitia maisha yako

Hao unao waona wamefanikiwa kwenye maeneo mbalimbali sio watu maalumu sana

Hawajaumbwa tofauti na wewe

Kila mmoja ana masaa 24 kama mwingine kwenye siku yake

Wote tuna damu na maji Sawa na akili Sawa tofauti ni matumizi ya akili tu

Ukiondoa tofauti za kimaumbile ambazo hazihusiani na kufanikiwa,

Mambo mengine yote tupo sawa

Hivyo wewe hukuletwa kushabikia mafanikio ya wengine,

Wala kujimbembelezesha kwa wengine au kusujudia wengine kisa wamefanikiwa

Wote tunapaswa kuheshimiana tu na kuhakikisha kuwa kila mmoja wetu anafanya kwa uwezo wake kile alicholetwa Dunia kufanya.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Kurudisha thamani iliyopotea

Next Post

Kurudisha thamani ya biashara yako

Acha Comment Yako

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.