You Can Win If You Want

Namna bora ya kujenga heshima katika jamii

Kwanini tunapaswa kujenga heshima? 

Kujenga heshima ni jambo la lazima lenye manufaa sana na umuhimu mkubwa kwa kila mmoja

kwani tabia zako ndio huwapa watu wote ishara kamili ya namna ulivyo kwenye maeneo yote

Nimekuandalia mbinu ambazo unaweza kutumia ili kujenga heshima katika jamii yote inayokuzunguka

Tumia mbinu hizi kujenga heshima katika jamii 

Kuwa na muonekano wenye heshima

kuanzia mavazi yako na namna unavyo tembea, jitahidi kuwa nadhifu muda wote hata kama juna mavazi ya aina nyingi

Vaa nguo zinazoendana na umri wako pia zinazoendana na mahala unapoenda

Kuwa msafi na jitahidi angalau kujikagua kabla hujatoka ndani ya chumba chako

Jiulize hivyo ulivyo vaa ikitokea ukakutana na mtu unae muheshimu sana utakuwa na uwezo wa kujiamini mbele yake?

Au mavazi uliyo vaa kama angevaa mtu mwingine je bado ungemuheshimu?

Lakini pia jiulize ukikutana na mtu kwa mara ya kwanza atapata tafsiri gani kupitia mavazi yako hata kabla  hujazungumza neno lolote?

Kujenga heshima kwa jamii

Chagua marafiki wenye heshima

Ndege wafananao huruka pamoja, huu ni msemo ambao unaaminiwa sana na jamii zetu

Hata kama upo tofauti na marafiki ulionao lakini huwa ni ngumu sana jamii kuamini kuwa hufanyi yale marafiki zako wanayo yafanya

Kama una marafiki wezi jamii huamini hata wewe ni mwizi, ukiwa na marafiki waasherati pia utaonekana muasherati

Hivyo epuka sana marafiki ambao hawana mipaka katika kulinda heshima zao ili na wewe uweze kuwa katika nafasi nzuri sana ya kuheshimika

Simamia majukumu yako ipasavyo 

Ili kulinda heshima yako jitahidi sana kusimamia majukumu yako ya maisha, kazi, familia na kila eneo lako ipasavyo bila kusukumwa au kulazimishwa

Kuwa mtu ambae upo makini na kila jambo linalokuhusu na lifanye kwa uhakika wa hali ya juu

Ili hata ikitokea bahati mbaya hujafanya basi watu wengine waelewe haraka tu kuwa ulipitiwa na utafanya bila shida

Watendee wengine vile unapenda wewe kutendewa

Hii ni pamoja na kuheshimu wengine bila kuchagua hali zako za maisha, umri wao, kazi zao, wala kitu kingine chochote

Chukulia watu wote ni Sawa na wanastahili kuheshimiwa hata kama uhalisia wa tabia zao haupo hivo

“Ukiheshimu wengine na wao watakuheshimu”

Jiwekee mipaka, heshimu mipaka ya wengine na jifunze kusema hapana

Usikubali kila jambo hasa kama lipo nje ya ratiba zako au uwezo wako, saidia watu kile unachoweza na sio kila wakati

Lakini pia weka taratibu zako na zifuate chagua mambo ya kushirikisha wengine na mambo yako binafsi na hakikisha hakuna anaevuka mipaka ya maisha yako

Na ikitokea mtu kavuka mipaka kemea mara moja kwa utulivu na hekima 

Lakini pia heshimu mipaka ya wengine na endapo hawapendwezwi wewe kuwa sehemu ya maisha yao jiondoe mara moja na usilamishe uhusiano aina yoyote

Jifunze kujitegemea ili kulinda na kujenga heshima yako

Kama umefikia umri wa kujitegemea maisha yako, fanya hivo mara moja

Hakikisha kuwa unasimamia majukumu yako ya maisha bila usaidizi kutoka kwa watu wengine tafuta kazi hata kama utaingiza kipato kidogo

Ikiwa  unaona bado huwezi kuishi mwenyewe usilazimishe sana ila wakati,

unajipanga kujitegemea onesha jitihada na saidia majukumu madogo madogo ya nyumbani

Ukikosewa usikae kimya onesha hisia zako na zungumza kwa heshima kukemea hilo

Usiwe mnyonge kiasi cha kuonekana mjinga kila mahala,

Kama umevunjiwa heshima usikae kimya kwa kuogopa cheo cha mtu au umri wa mtu

lakini pia usianzishe ugomvi wala kujibu kwa hasira badala yake mfate pembeni aliyekukosea na zungumza nae kwa nia njema

Jipende na onesha upendo kwa wengine

Hakikisha kuwa unaanza wewe kujipenda na kisha penda watu wote bila kuchagua wala kufanya upendeleo,

Chukulia kila mmoja kama unavyojikulia wewe na jitahidi sana kufanya watu wawe huru wanapokuwa na wewe kwa kuzungumza nao bila kuonesha dharau wala majivuno

Epuka ahadi za uongo na tabia za udanganyifu

Siku zote usiahidi kitu ambacho huwezi kutimiza hata kama ni kidogo,

Kwani watu huwa na tabia ya kutunza kumbukumbu na ikitokea mara kadhaa umeahidi na hujatekeleza basi hukuweka katika kundi la watu waongo

Pia usiwe mtu wa kudanganya danganya mara kwa mara japokuwa kuna muda uongo husaidia kuweka mambo Sawa Ila isiwe kila nyakati

Tumia uongo pale tu inapobidi na pale ambapo ukweli hauwezi kuweka mambo Sawa

Usiongee sana na kuwa wa mwisho kuzungumza

Jitahidi kulinda heshima yako kupitia ulimi wako, kwani kimtokacho mtu mdomo mwake ndicho kilichomjaa moyoni mwake

Kumbuka kauli huwa hazirudi nyuma, hivo kitu kikubwa zaidi katika heshima ni kauli zako

Bora ujulikane kwa kutoongea kuliko kujulikana kama muongeaji ambae hana heshima kwa kauli zake

Jitahidi kusikiliza wengine kwanza kisha wewe toa maoni mwishoni,

Itakusaidia kuzungumza kile ambacho wengine wamekisahau na kukufanya uonekane una akili nyingi

Sikiliza wengine na wape nafasi

Usiwe mtu wa kuona mawazo ya wengine hayana maana hata kama umewazidi akili, cheo au uchumi

Siku zote jua kuwa hakuna mkamilifu na kila mtu ana mawazo tofauti na mwingine hivo kuwapa nafasi wengine husaidia kujenga kitu bora zaidi

Zuia hisia zako

Kuna aina nyingi za hisia kama huzuni, hasira, furaha na nyinginezo,

Ili kulinda heshima yako hakikisha kuwa una chagua aina ya hisia ya kuionesha mbele za wengine

Hususani hisia mbaya kama hasira kwasababu huweza kukupelekea kufanya jambo ambalo litakuvunjia heshima yote uliyo jenga miaka yote

Jitokeze na onekana kwenye matukio muhimu na toa ushirikiano

Matukio kama misiba, harusi, sherehe mbali mbali husaidia sana kujenga na kulinda heshima yako katika jamii inayokuzunguka

 Ni vizuri kuhudhuria na unapokosa muda toa kudhuru yako mapema

Lakini kujenga heshima ni pamoja na kushirikisha katika kazi mbali mbali sio kufika na kukaa tu bila kusaidia wengine pale unapoweza

Kubali makosa na omba msamaha

Hakuna binaadam ambae hakosei kwani hakuna mkamilifu, hivyo unapogundua umekosea hakikisha kuwa una kiri kosa lako na kuomba msamaha wa dhati

kisha haraka rekebisha makosa yako hata kama umemkosea mtoto wako au mtu unae mzidi umri na cheo

Epuka ugomvi ili kujenga heshima yako nzuri

Waswahili wanasema muungwana akivuliwa nguo huchutama

Kuna nyakati utakutana na maudhi mengi sana na ambayo yatakupelekea hasira na kutamani kugombana au kurushiana maneno

Hata kama kweli umekosewa jitahidi kuwa na busara na kamwe usigombae na mtu kwa sababu zozote zile

Ukiona jambo ni kubwa na haliwezekani kutatuliwa kwa mazungumzo basi fata sheria

Ugomvi ni adui mkubwa wa heshima hivo jitahidi na kuwa makini sana

Tumia mitandao ya kijamii vizuri 

Epuka kutukana, kujibizana, au kuchangia maudhui yasiyofaa mitandaoni hata kama huoneshi sura yako

Kumbuka dunia hii ni ndogo sana na kuna siku lazima kila jambo litakuwa wazi na hivo kushushia kabisa heshima yako

Mtandao kama jamiiforums ni sehemu nzuri sana ambayo mtu huweza kujifunza na kuchangia chochote bila kuonesha sura wala jina halisi,

Hii huwapa watu nafasi ya kuandika mambo yasiyofaa kwakua wana uhakika wa siri zao kutokuwa wazi

Na kusahau kuwa mitandao inatunza kumbukumbu na kuna siku mambo yanaweza kwenda kombo na kuwa wazi hivo kuleta madhara katika heshima yako nzima

Omba msaada

Ukitaka wengine wa kuheshimu zaidi basi waombe msaada hata kama ni Msaada kidogo,

Kwani hakuna ambae hahitaji msaada kabisa kwenye maisha, hata kama una pesa nyingi kuna wakati utahitaji watu wengine wakusaidie mambo kadhaa

Jambo hili litafanya jamii na wanaokuzunguka kufurahia na kuona kuwa hata wao wana umuhimu katika maisha yako.

Hitimisho 

Nimuhimu kulinda heshima zetu kwani maisha ni mafupi sana na hatujui kesho yetu itakuwaje

Unae mdharau leo kesho huenda akawa Msaada wako mkubwa kesho 

Hivo inatupasa tujifunze kuwa maisha hayana kanuni maalumu na tusidanganywe na mali, vyeo, familia na hata afya za sasa.

pia soma mafanikio.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Faida za kuanza biashara kwa mtaji mdogo

Next Post

Mbinu za kusahau mambo ya nyuma na kuanza maisha mapya

Acha Comment Yako

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.