You Can Win If You Want

Mambo ya kuzingatia kukuza biashara yako

Kukuza biashara inahitaji mbinu mbalimbali za kuzingatia kila siku na kila wakati

Biashara zote zinahitaji mikakati na mipango ili kuweza kuendelea kusimama imara sokoni

Hivyo nimekuandalia mbinu kadhaa zinazoweza kukusaidia kukuza biashara yako  yoyote

Mbinu za kukuza biashara

Mbinu za kukuza biashara

wazo bora

Anza kuwa na wazo bora ambalo linaendana na,

  1. Uhitaji, uwe na uhakika kuwa wazo la biashara yako linauzika! yani fanya utafiti wakutosha hata kabla hujaanza biashara na wazo na wazo linalojiuza lenyewe
  2. Ushindani mdogo, Angalau jihakikishie kuwa hakuna biashara au huduma nyingi zinazoendana na wazo la biashara yako kwanza

Ubora wa bidhaa au huduma

Hata kama kuna ushindani mkubwa basi angalau uwe na huduma na bidhaa bora ambazo zinatatua changomoto za mteja moja kwa moja

Jifunze kujitofautisha kwa washindani wengine, yani usikubali washindani wakuzidi maarifa!

Chunguza wateja wanataka nini na weka zaidi ili kukuza biashara yako

Mfano zingatia

  1. Punguzo la bei
  2. Ofa mbalimbali kama, vifungashio vya bure au free delivery nk
  3. Zawadi mbalimbali kwa wateja nk

Lakini pia kwenye ubora wa bidhaa zingatia

  1. Bidhaa zinatatua changomoto za wateja moja kwa moja
  2. Zinadumu muda mrefu
  3. Zina leta hisia za kipekee kama harufu nzuri ya tofauti
  4. Rahisi kutumia
  5. Haimuingizi mteja gharama za ziadi nk

Yani wewe mwenyewe jiulize kitu unachokifanya kama ungekuta mtu mwingine anauza ungeweza kukinunua? Au ungerudi tena kununua?

Chapa bora ya biashara (branding)

Jitahidi kuwa biashara yako iwe na Chapa (brand) ya kipekee

Kiasi kwamba mteja hata kama atanunua kwa mara ya kwanza basi asikusahau na akumbuke kila anapotaka kununua tena

Hapa zingatia Haya

  1. jina la bidhaa/huduma yako
    Usiweke jina gumu sana wala refu sana, lisiwe jina lenye maana mbaya wala maana isiyoendana na biashara unayofanya, usiige jina la biashara ya mtu mwingine
  2. logo
    Zingatia uwe na logo nzuri na nyepesi unayotumia kwenye biashara yako hata kama Biashara Ni ndogo, hii itasaidia mteja kukukumbuka haraka na inasaidia kujitofautisha hasa unapotangaza biashara yako mitandaoni
  3. Rangi
    Weka rangi nzuri za kuvutia kwenye biashara yako kuanzia kwenye ofisi au duka, logo, majarida, kadi za biashara, bidhaa zenyewe na hata kwenye matangazo hapa itafanya mteja akiona rangi fulani kama anahitaji huduma au bidhaa kama yako kwa wakati huo biashara yako itamjia kichwani
  4. Mfumo mzima wa huduma na bidhaa zako za biashara
    Tengeneza ladha yako, kuanzia kwenye namna unavyo pokea mteja, vifungashio, aina ya salamu unayotumia, namna unavyoongea nao, masaa ya kufungua na kufunga biashara yaendane siku zote nk

Yani kichwani kwa mteja ajue kabisa muda gani kila akija anakuta upo wazi,

Ategemee nini pale apoingia mapokezi, atarajie nini wakati anapata huduma yako nk

Hii hufanya mteja kukariri na hata kuwapa  urahisi kushawishi wengine wenye uhitaji wa na bidhaa au huduma yako hivyo kusaidia kukuza biashara yako

Masoko na mauzo 

Hapa sasa ndio sehemu muhimu kwa biashara yoyote, hata kama huko juu umeharibu ila hapa ndio moyo wa biashara

Hakikisha kuwa biashara yako inatangazwa na unajitangaza kila siku!
“biashara ni matangazo”

Kumbuka hata kampuni kubwa kama Coca-Cola kila siku unakutana na matangazo yao

Ijapokuwa ni bidhaa inayojiuza, ipo dunia nzima na ina soko la uhakika

Hivyo lazima ujitangaze hata kama Biashara yako imeshakuwa kubwa

Kila siku  jitahidi kutafuta mbinu mbali mbali za kuonekana katika soko

Tumia njia kama

  1. Magazeti na majarida
  2. Email na bulk sms
  3. Redio na Television
  4. Mitandaoni kama Instagram na Facebook na lipia ads kwa gharama unayoweza
  5. Mabango ya barabarani
  6. Semina za biashara, nenda na bidhaa au huduma yako na jitangaze
  7. Ingiza bidhaa na huduma mitaani na ongea na wateja uso kwa uso

Hapo utachagua namna ya kujitangaza kulingana na uwezo wako

Lakini njia rahisi zaidi ni mitandaoni kama Facebook na Instagram

Hii unaweza fanya bure tu kwakuwa na Akaunti yako maalumu ya biashara yako na utapata wateja wengi sana

Lakini pia kwenye kipengele cha masoko na mauzo hakikisha

  1. Una bidhaa inayojiuza
  2. Namna bora ya ushawishi kwa wateja (lugha nzuri na laini inayoshawishi)
  3. Timu bora ya wauzaji
    hapa kama Biashara yako ni kubwa tafuta watu wenye mafunzo imara waingie mitaani na huduma au bidhaa zako wakiwa na sare zenye nembo ya biashara

Kama huna watu (team) na biashara ni ndogo basi ingia mwenyewe sokoni

Usingoje wateja wakufate ulipo! Andaa kadi za biashara (business cards) au vipeperushi

Kila unaehisi  anaweza kuwa mteja muachie kadi yako ya mawasiliano

Huduma kwa wateja 

Hapa zingatia kuwa mteja anaridhika na huduma au bidhaa kuanzia anavyopokelewa mapokezi au kwenye simu

  1. Mteja ahudumiwe haraka na kwa ubora mkubwa
  2. Majibu mazuri kwa wateja (Kauli) kumbuka “mteja hakosei ” hivo mteja lazima abembelezwe
  3. Kama unafanya biashara yako mtandaoni hakikisha una jibu wateja kwa wakati na waridhike na kile wanachosikia, usikubali mteja akate simu bila kuona kama amerdhika

Uongozi na usimamizi mzuri

Hapa sasa angalia namna unavyo simamia wafanyakazi wako

Usiwe mpole sana wala mkali sana

Kuwa kiongozi ambae anajua namna ya kufanya wafanyakazi wawajibike wenyewe bila kusukumwa

Wafanyakazi wakiridhika lazima watahudumia wateja vizuri na biashara itakuwa

Wafanyakazi wakikosa mapenzi na kazi yao basi biashara lazima itakufa tu hivyo zingatia

  1. Sikiliza wafanyakazi wakueleze changamoto zao za kazi na zifanyie kazi haraka
  2. Wape Nafasi ya kutoa maoni mara kwa mara kwenye biashara
  3. Kuwa na Kauli za kibinadam na utu kwa wafanyakazi wote na usibague wala kupendelea
  4. Wape motisha hasa wale wanaofanya vizuri katika maeneo mbali mbali ili wazidi kufanya zaidi na wale wengine wapate hamasa
  5. Kuwa muwazi hasa katika mambo ya biashara kwa kuweka vikao vya mara
  6. Wape elimu na mafunzo ya mara kwa mara

Kumbuka kuweka vikao mara kwa mara,  kuwasikiliza na kushirikisha kinachoendelea ili kurekebisha mambo mapema

Usimamizi mzuri wa fedha

Hapa ndio kama roho ya biashara ili ikue

Lazima ujue namna ya kusimamia fedha za biashara kwa,

  1. Kudhubiti matumzi ya biashara yako ya kila siku
  2. Kupunguza na kuondoa mambo yasiyo ya lazima sana
  3. Kutofautisha matumzi ya binafsi na matumizi ya biashara
  4. Kuongeza bidhaa na kununua mapungufu yote kwanza kabla ya matumizi
  5. Kuhakikisha kuwa biashara inajikuza kupitia faida yake yenyewe

Uvumilivu na Uendelevu

Hakuna biashara inayokuwa mara moja, biashara ni kama mbegu ya zao lolote,

Laizma upande mbegu, uizingatie kwa kuihudumia vizuri ili ikuwe

Na pia kuanza kula matunda ya biashara inataka uvumilivu mkubwa

Usiwe na haraka wala tamaa biashara zote zinapitia changamoto!

Jitahidi kuwa na subra na uwe na malengo ya muda mrefu katika biashara yako.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Changamoto za biashara na jinsi ya kukabiliana nazo

Next Post

Kurudisha thamani iliyopotea

Acha Comment Yako

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.