You Can Win If You Want

Kurudisha thamani iliyopotea

Utawezaje kurudisha thamani yako ?

Kurudisha thamani iliyopotea huweza kuwa jambo lenye changamoto kubwa kutokana na ugumu wa chanzo au hata mazingira

Thamani inaweza kupotea kutokana na sababu mbali mbali za kila siku

Kuna makundi mengi yanayohusiana na upotezaji wa thamani

Thamani inaweza kupotea kwa mtu binafsi, familia hata biashara.

Leo tutaangalia thamani ya mtu binafsi  na njinsi ya kurudisha baada ya kupotea

Dalili za kupotea kwa thamani ya mtu

  1. Kuvunjika kwa heshima na kudharaulika
  2. Kupoteza mvuto
  3. Msongo wa mawazo na kuelemewa
  4. Kutosikilizwa
  5. Kutokubalika
  6. Kutopewa kipaombele
  7. Kupoteza muelekeo wa maisha
  8. Kupoteza watu wa karibu
  9. Kukosa Msaada wa haraka

Kurudisha thamani iliyopotea

Kupotea heshima

Utajua kuwa thamani yako imeshuka kwa kuona  hali ya kuogopwa Inaondoka na kila mtu aliyekuwa anahisi uwepo wako kama awali inaisha kabisa

Utaanza kuona mabadiliko kwa watu wako karibu kama watoto, mwenza, ndugu hata jamii

Watafanya mambo mengi mabaya hata usiyoyapenda mbele yako!

Hakuna anaekujali tena na unaonekana kama haupo mbele yao

Ukiongea kitu, kuomba kitu au kuuliza kitu hutopata kwa haraka au usipate kabisa.

Kupoteza mvuto

Ile hali ya kupendwa uliyokuwa unaihisi mwanzo inaisha

Unaona hakuna tena hisia kati yako na wanaokuzunguka

Hata mke /mume wako, watoto na watu wengine hawakupendi tena na wanakuona mtu wa kawaida kama mtu asiye na maana yoyote kwao.

Msongo wa mawazo

Utaanza kuhisi hali ya kuelemewa sana

Hii hutokana na mabadiliko mengi unayokutana nayo ambayo hukuzoea awali

Inaweza kuwa kazini au nyumbani

Utajikuta kama kuna kitu hakipo Sawa kwenye mwili au moyo wako

Japokuwa kwa mazingira ya nje unaona mambo yanaenda vile vile

Ila kwa upande wako unahisi kabisa kuna mambo yamepungua katika maisha yako ya kila siku

Hii hupelekea kufanya mambo mengi kwa hasira na kuchanganyikiwa mara kwa mara.

Kutokusikilizwa

Hapa utaona kama kila unacho ongea kina puuzwa

Iwe kazini hata nyumbani! Watu hawana muda na maneno yako tena

Hata ukijitahidi kuonesha kuwa upo sahihi hakuna atakae kujali

Hata kama utakuwa sahihi kweli!

Kutokukubalika

Hapa utaona hali ya kutengwa na kuonekana kama nuksi kwa wengine

Iwe mke /mume, watoto, marafiki nk

Utajihisi kabisa hali ya kuwekwa nyuma kwenye mambo mengi

Hutoshirikishwa katika mambo muhimu ambayo mwanzo ulipewa kipaombele

Hutoambiwa vitu vya msingi wala vitu vya furaha kwa wengine

Mara nyingi utajiona kama mtu wa kujipendekeza kwa watu.

Kupoteza muelekeo wa maisha /watu wa karibu na kukosa Msaada wa haraka

Hapa sasa utaona unakosa ramani za maisha yako

Utajihisi kama watu wa karibu yako wametafuta watu wengine

Utajina kama huna maana tena wala huna Msaada wowote unaouhitaji kwa haraka.

Sababu/chanzo cha kupoteza thamani
Tabia

  1. Tabia
  2. Changamoto za mara kwa mara
  3. Kuishi kwa mazoea
  4. Sababu za kiasili
  5. Kuyumba kimaisha
  6. Kutoheshimu /thamini wengine
  7. Kutosimamia majukumu yako ipasavyo

Tabia

Hapa kuna tabia kama za ulevi, matusi, kejeli, ugomvi dharau nk

Tabia hizi husababisha mara nyingi watu wa karibu yako kukuchoka

Kuna muda watu hukuvumilia kwa kuamini utabadilika,

Lakini muda mrefu ukipita bila kuona mabadiliko huanza kukuzoea na mwisho kuku dharau na kukucha kabisa!

Changamoto za mara kwa mara

Hapa kuna zile changamoto za maisha ya kila siku

Hufanya watu kuchoka shida zako

Kila wakat kulalamika, kuomba misaada, kutegemea wengine na hata kusimulia matatizo yako

Watu huchoka na kuona hawaoni furaha ya maisha yao mengine zaidi ya shida zako

Yani wengi hukupenda pale na wewe una furaha binafsi na unawapa furaha wao

Asilimia kubwa ya watu hawapendi kusikia matatizo ya wengine na husikiliza kwa kejeli tu.

Kuishi kwa mazoea

Hali ya kila siku kuishi kama jana!

Hubadiliki wala kukubali mabadiliko

Kila siku unaishi maisha ya mazoea wakati wengine wanatafuta namna ya kuanza upya na kuboresha mambo yao

Hufanya watu kukuchoka na kukuona kama mzigo!

Hata kama ni mwenza wako au watoto epuka kuzoeleka

Yani ishi maisha ya mtu asijue ukirudi utakuja na nini au ratiba gani.

Sababu za kiasili

Kuna nyakati hufika za watu kuondoka katika maisha yako na wewe kupoteza thamani kwao

Nyakati hizi ni pale hujafanya kosa lolote

Hujawaudhi wala kuvuka mipaka

Lakini bila kujua chanzo unashangaa tu Huna tena thamani mbele yao!

Kuyumba kimaisha

Mfano kufirisika au kupoteza kazi

Uchumi wako ukitetereka lazima na wewe thamani yako ishuke

Wengi huja katika maisha yako sababu kuna kitu wanapata kutoka kwako!

Inawezekana hata huyo mke au mume wako na marafiki wapo na wewe sababu za pesa zako!

Au kuna kitu wanategema utawasaidia

Na siku wakiona huna tena kile wa nachotaka kutoka kwako  hukushusha thamani yako yote.

Kutoheshimu!/kutothamini wengine

Kuna ile hali ya mtu kuona wengine kama hawana maana kwao!

Hii husababishwa na Elimu, Mali na pesa

Hivo watu huzoea hio hali na baada ya muda hukuchukulia kawaida kwao.

Kutosimamia majukumu yako ipasavyo

Mfano kutohudumia familia kama chakula, mavazi, ada nk

Kutowajibika kama mke au mume

Kutowajibika katika jamii inayokuzunguka

Kutojua nafasi yako na majukumu yako ya kazi na,

Kutofanya kazi zako inavyotakiwa hupelekea hali ya kuchokwa na kushuka kwa thamani yako!

Usaliti wa mara kwa mara

Hii huwa chanzo kikubwa hasa kwa wanandoa na marafiki

Hali ya kuanzisha mahusiano ya kimapenzi au kirafiki na watu wengine tofauti na mwenza wako au rafiki yako wa dhati

hupelekea maumivu makali kwa mwenza wako na rafiki aliye kuamini sana

Na baada ya muda huamua kushusha thamani kwenye moyo na maisha yake!

Utegemezi

Sana kwa wale ambao hawana kazi na hawataki kujishughulisha kwa lengo la kujisimamia katika majukum yao

Kuna watu hupenda kuishi kwa kutegemeana wenzao kwa kisingizio cha hana kazi!

Hii husababisha baada ya muda kuchokwa na kudharaulika mwisho wa siku kushuka kwa thamani yako.

Hatua za kurudisha thamani iliyopotoea
Kubali thamani yako imeshuka

  • Kubali thamani yako imeshuka
  • Tafuta chanzo
  • Weka mikakati na badili tabia
  • Usitumie nguvu kubwa ya maneno fanya kwa vitendo
  • Jipe muda
Kubali thamani yako imeshuka

Usilazimishe kujipa thamani kwa watu ambao tayari hawakuthamani

Itafanya wazidi kukuzarau!

Kubali hali yako iliyopo kwa wakati huo na itakusaidia kukupa mwanga wa kutibu tatizo na kurudisha thamani iliyopotoea.

Tafuta chanzo

Huwezi kutibu tatizo bilaa kujua chanzo

Anza kutafuta kwanini hauthaminiki tena? Ili ujue namna ya kuondoa tatizo kwanza

Mfano labda ni tabia za usaliti, ulevi na hata uongo.

Weka mikakati na badili tabia

Baada ya kujua chanzo cha kushuka kwa thamani yako

Sasa jiulize ufanye nini ili upandishe thamani!

Badili kila kitu ambacho kilipelekea wengine kukudharau

Jiwekee malengo ya mabadiliko yako binafsi

Amua kuwa mtu mwingine kwa faida yako mwenyewe kwanza.

Usitumie nguvu kubwa

fanya kwa vitendo

wala usiongee kitu, kuwa unataka kubadilika nk

Maana utawafnya wakuone mjinga zaidi

Wewe Fanya kwa vitendo tu halafu acha wenyewe waone mabadiliko yako.

Jipe muda

Kumbuka hauthaminiki tena! Huna mvuto wala ushawishi

Kwahio itataka muda wa kutosha kuaminisha wengine na wajiridhishe kuwa umebadilika

Hivo hupaswi kamwe kufanya kwa haraka

Endelea taratibu kufanya mambo yako mpaka pale hali itakaporudi kama zamani

Na kuna muda hali inaweza usiweze kurudi na kuwa kama zamani

Yani thamani iliyopotoea kuna muda hairudi kama awali kwahio punguza matarajio.

Njia mbalimbali za kurudisha thamani iliyo potea

  • Jitegemee na tafuta kazi
  • Jipende wewe kwanza na jipe kipaombele
  • Heshimu na thamini wengine
  • Simamia majukum yako ipasavyo
  • Epuka tabia mbaya kama ulevi, uzinzi nk
  • kuwa muaminifu kwa wengine
  • Weka mipaka ya maisha yako
  • Kuwa msiri na Epuka kulilia watu shida zako au kuomba misaada ya mara kwa mara
Jitegemee au tafuta kazi

Epuka kukaa nyumbani kwenu au kwa ndugu yako yoyote bila kazi

Ikiwa umeshatimiza umri wa kujitegemea hasa kama ni mtoto wa kiume

Na kama kuna ulazima wa kukaa kwa ndugu zako basi angalau changia mahitaji madogo madogo.

Jipende wewe kwanza na jipe kipaombele

Epuka kuishi kwa mazoea!

Anza kujipa thamani kwa kujipenda mwenyewe kabla wengine hawajakupenda

Jipe furaha, vaa pendeza, jitoe sehemu mbalimbali na jiheshimu

Ukiwa mtu unaejijali basi wengine pia watakuja na kukupenda  na itakusaidia kurudisha thamani iliyopotoea.

Heshimu na thamani wengine

Kama jinsi unataka wewe kuthaminiwa

Basi lazima pia uthamini wengine!

Usitegemee kuthaminiwa ikiwa unadharau wengine hata kama umewazidi kila kitu.

Simamia majukumu yako ipasavyo

Hakikisha kuwa kila jukumu linalokugusa unasimama nalo

Usiwe mtu wa kutegea wengine wakusaidie yale uliyopaswa kufanya wewe

Kuanzia majukumu ya familia mpaka kazi lazima uyafanye kwa uhakika wote bila kusukumwa au kupigiwa kelele.

Epuka tabia mbaya ni njia nzuri ya kurudisha thamani iliyopotoea

Tabia kama ulevi, uzinzi, uasherati na ugomvi ni chanzo kikubwa cha kudhaurika

Jitahidi uwe na adabu binafsi na kwa watu wanaokuzunguka

Heshimu Kauli zako na usiwe mtu wa kuyumbishwa yumbishwa.

Acha usaliti!

Ikiwa umemsaliti mtu jua kabisa hawezi kukuamini tena

Na itafika muda atakutoa katika moyo na kukushusha thamani

Jitahidi kuwa muaminifu ili uaminiwe pia.

Weka mipaka ya maisha yako

Jitahidi sana watu wasikuzoee kupitiliza

Jiweke mipaka na usikubali watu waivuke

Hii iambatane na kusema hapana kwa vitu ambavyo vipo kinyume na wewe

Pia heshimu mipaka ya wengine.

Kuwa msiri na epuka kuomba misaada ili kurudisha thamani iliyopotoea

Misaada ya mara kwa mara huchosha na kufanya wengine kukudharau

Jitahidi kutunza shida zako na kuzitafutia ufumbuzi wewe mwenyewe bila kuhusisha wengine

Itakusaidia sana kujenga na kurudisha thamani iliyopotoea

Maana hata wengine pia wana shida zao.

Share this article
Shareable URL
Prev Post

Mambo ya kuzingatia kukuza biashara yako

Next Post

Kiwango cha umasikini na hamasa

Acha Comment Yako

Read next

Huruhusiwi ku copy. Asante.